RAIS SAMIA AFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA



   Mapema leo Ikulu, jijini Dar es Salaam nimekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa vyama vya siasa hapa nchini ikiwa ni sehemu ya kuendeleza utamaduni wa mawasiliano, mashauriano na ushirikiano katika masuala muhimu yanayolihusu Taifa letu. 


Mazungumzo haya ni fursa ya kubadilishana mawazo na mitazamo mbalimbali kwa maslahi mapana ya Taifa, huku tukiendelea kujenga msingi wa kuheshimiana, kuelewana na kushirikiana. 


Serikali itaendelea kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali wa kisiasa katika kulinda amani, kudumisha umoja wa kitaifa na kusukuma mbele maendeleo yenye manufaa kwa Watanzania wote.


 

0 comments: