Wakuu wa Tanzania wanasema sasa inajulikana kuwa watu 18 walikufa wakati jengo moja lilokuwa likijengwa lilipoporomoka mjini Dar es Salaam.

Jengo liloporomoka kati-kati ya mji wa Dar-es-salaam


Watoto wawili ni kati ya maiti zilizopatikana.

Kazi ya uokozi inaendelea lakini hakuna matumaini ya kunusuru maisha.

Watu kadha bado wametoweka.

Jengo hilo la ghorofa kadha lilikuwa kati-kati ya mji.

Waandishi wa habari wanasema ujenzi wa majumba umeongezeka Tanzania kwa sababu ya uchumi kukuwa, lakini kuna wasi-wasi kuwa vigezo vya ujenzi havifuatwi.

0 comments: