MADAKTARI BINGWA WA MOI KWA KUSHIRIKIANA NA MADAKTARI BINGWA HOSPITALI YA NYANGAO MKOANI LINDIA WAWAFANYIA UPASUAJI WAGONJWA 1500

 
Mkurugenzi mtendaji wa MOI, Dkt Respicious Boniface akizungumza jambo mara baada ya Upasuaji Mkoani Lindi.
  Madaktari wakiendelea na Upasuaji 
Mkurugenzi mtendaji wa MOI, Dkt Respicious Boniface (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa hospitali ya Nyangao Lindi pamoja Mganga mkuu wa Wilaya ya Mtama.

Na Mwandishi Wetu,

Wagonjwa zaidi ya 1,500 wamefanyiwa upasuaji na madaktari bingwa wa MOI katika hospitali ya Nyangao Mkoani Lindi  kipindi cha miaka mitatu toka Taasisi ya MOI ilipoingia mkataba wa ushirikiano na hospitali hiyo ili kusogeza huduma za kibingwa kwa wananchi wa Mikoa ya Kusini.

Kutokana na uwepo wa huduma za kibingwa za mifupa katika hospitali ya Nyangao, Serikali imeweza kuokoa zaidi ya Tsh Bilioni 2.7 ambazo zingetumika kusafirisha wagonjwa hao kufuata matibabu Dar es Salaam.

Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mh Shaibu Ndemanga ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mh Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajali wananchi wa mikoa ya kusini kwa kuwasogezea huduma za kibingwa za Mifupa na kuwaondolea  adha ya kuzifuata huduma hizo MOI.

“Naomba nianze kwa kuishukuru Wizara ya Afya kwa kazi kubwa, Pia Kwa namna ya pekee naomba niishukuru Taasisi ya MOI ikiongozwa na Dkt. Respicious Boniface  kwa kutekeleza kwa vitendo agizo la Serikali la kusogeza huduma za kibingwa kwa wananchi hususani katika mkoa wetu wa Lindi na kuwapunguzia  gharama wananchi, jambo hili limewajengea imani kubwa  wananchi kwa  Serikali ” Alisema Mh. Ndemanga

Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Mtama, Bw. George Mbilinyi amesema uwepo wa huduma za kibingwa za mifupa za MOI katika hospitali ya Nyangao umepelekea wagonjwa kutoka mikoa ya Mtwara, Lindi, Ruvuma na mataifa jirani ya Msumbiji, Comoro na Malawi kufika hospitalini hapo ili kupata huduma.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt.Respicious Boniface amesema Taasisi ya MOI itaendelea kusogeza huduma zake karibu na wananchi ambapo hivi karibuni huduma za kibingwa za mifupa za MOI zitaanza kutolewa katika hospitali ya rufaa ya kanda ya kusini Mtwara .

“Tunashirikiana na wenzetu wa KCMC katika huduma za Ubongo na mishipa ya fahamu, tunashirikiana na wenzetu wa Bugando katika huduma za upasuaji wa magoti kwa njia ya Matundu, tunashirikiana na wenzetu wa Benjamin Mkapa katika upasuaji wa Nyonga na Magoti lengo letu ni kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi huko walipo kama Serikali inavyoelekeza” Alisema Dkt. Boniface.

Akitoa shukrani kwa niaba ya uongozi wa Hospitali ya Nyangao, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mtama Dkt. Dismas Masulubu ameishukuru Taasisi ya MOI kwa kuanzisha ushirikiano na Hospitali ya Nyangao ambapo wagonjwa wamekua wakipata huduma za kibingwa bila kulazimika kuzifuata huduma hizo Dar es Salaam.

0 comments:

WATAALAM WA AFYA NCHINI WAPATIWA MAFUNZO YA KIMATAIFAA JINSI KUFANYA KIPIMO CHA MOYO KWA KUTUMIA MASHINE YA ECHOCARDIOGRAM (ECHO)

  Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo na utafiti wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akielezea namna mafunzo ya Echo yatakavyofanyika kwa washiriki wa mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwakutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yanayoendelea katika Taasisi hiyo iliyopo Jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) 
Mbunge wa viti Maalum Mhe. Dkt. Alice Kaijage akielezea ujuzi atakaoupata katika mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yatakavyomsaidia katika taaluma yake wakati wa mafunzo hayo ya siku mbili yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Jijini Dar es Salaam.
   Mbunge wa viti Maalum Mhe. Dkt. Alice Kaijage akielezea ujuzi atakaoupata katika mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yatakavyomsaidia katika taaluma yake wakati wa mafunzo hayo ya siku mbili yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo Jijini Dar es Salaam.
   Daktari bingwa wa magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Piedmont Health iliyopo Atlanta Georgia nchini Marekali Dkt. Mani Vannan akiwafundisha watalaam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini namna ya kupima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam.
   Wataalam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na mkufunzi kutoka Taasisi ya Piedmont Health iliyopo Atlanta Georgia nchini Marekali Dkt. Mani Vannan ya namna ya kupima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam.
Wataalam wa afya kutoka hospitali mbalimbali nchini wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na mkufunzi kutoka Taasisi ya Piedmont Health iliyopo Atlanta Georgia nchini Marekali Dkt. Mani Vannan ya namna ya kupima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) wakati wa mafunzo hayo yanayoendelea katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yanayoendelea katika Taasisi hiyo Jijini Dar Es Salaam. Mafunzo hayo yaliyoudhuriwa na wataalam wa afya zaidi ya 100 yamefanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini.


Na: Genofeva Matemu – Dar es Salaam

19/08/2022 Wataalam wa afya zaidi ya 100 kutoka hospitali binafsi na hospitali za umma wameshiriki mafunzo yakimataifa ya siku mbili ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) ambayo yamefanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini.

Akizungumza na waandhishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi alisema kuwa mafunzo hayo yanatolewa na wakufunzi na wabobezi wakuu wa magonjwa ya moyo kutoka nchini Marekani.

Prof. Janabi alisema kuwa lengo la mafunzo hayo nikuongeza ujuzi kwa wataalam wa afya ili kusaidia na kupunguza wagonjwa ambao wanaingia gharama kutoka mikoani kwenda JKCI kwa ajili ya kufanyiwa kipimo cha Echo kwani wakiweza kuwagundua katika maeneo yao ya kazi wataweza kuchagua wagonjwa wanaohitaji kufanyiwa matibabu zaidi na kuwatuma JKCI.

“Tumekua tukifanya mafunzo kama hayo huko nyuma lakini kwa kutumia wataalamu wetu wa ndani ndio maana leo tunasema haya ni mafunzo yetu ya kwanza yakimataifa kwasababu tuna wabobezi na wataalam zaidi katika uchunguzi wa jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO) kutoka nchini Marekani”,

“Kwetu sisi wataalam wakutoa huduma za matibabu ya moyo, hatuwezi kufanya upasuaji wa aina yoyote bila kufanya kipimo cha Echo hivyo ujuzi tutakaoupata hapa utasaidia zaidi kuboresha huduma zetu na  kuchagua wagonjwa wapi waende kwenye upasuaji na wangapi wanaweza kutumia dawa bila ya kufanyiwa upasuaji”, aliseama Prof. Janabi

Prof. Janabi alisema kuwa mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanyakazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) yataendelea kutolewa kila mwaka kwa wataalam wote wa afya bila kubagua waliopo katika hospitali za umma na zile za binafsi ili kujifundisha mbinu mpya za kugundua matatizo ya moyo awali kabla ya tatizo kuwa kubwa.

Mshiriki wa mafunzo hayo ambaye ni Mbunge wa viti maalum Mhe. Dkt. Alice Kaijage alisema kuwa ameshiriki mafunzo ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO) ili aweze kupata mbinu mpya na zakisasa katika kutoa huduma za matibabu ya moyo.

“Nikiwa bungeni tuna kituo cha afya hivyo kwanjia moja ama nyingine naweza kusaidiana na wenzangu kama mtaalamu kupima moyo unavyofanya kazi kwa wagonjwa wanaofika katika kituo hicho lakini pia kupitia taaluma yangu natakiwa kuongeza ujuzi ili niweze kuendana na maendeleo ya sayansi na teknolojia”

Kwa upande wake Mkufunzi kutoka Taasisi ya Piedmont Health iliyopo Atlanta Georgia nchini Marekali Dkt. Mani Vannan alisema kuwa anaamini katika mafunzo ya mara kwa mara katika taaluma ya afya na nimoja ya matamanio yake kuona wataalam wa afya wanashiriki mafunzo ya kuongeza taaluma zao kila wanapopata fursa.

“Naamini Taasisi hii inamisingi mizuri katika taaluma ya upimaji wa jinsi moyo unavyofanya kazi kwa kutumia mashine ya Echocardiogram (ECHO), madhumuni ya mafunzo haya nikuifanya nchi hii kuwa kituo cha ubora katika utoaji wa huduma za kibingwa za vipimo na matibabu ya moyo”, alisema Dkt. Mani

Naye Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tiba Shirikishi katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Delila Kimambo alisema kuwa kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanyakazi ni moja ya huduma za tiba shirikishi ambayo nimuhimu kwa mtaalam wa afya kujua matatizo aliyonayo mgonjwa na kumpa mwelekeo wa huduma gani mgonjwa anastahili kupewa.

“Mgonjwa yeyote wa moyo nilazima afanyiwe kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO), ni kipimo muhimu ambacho wataalam waliopo hapa leo wanapaswa kukifahamu kwa undani zaidi ndio maana tumeandaa mafunzo haya ili tuwakumbushe na kuwafundisha waweze kutoa huduma hiyo katika ubora zaidi”,

“Unapofanya kipimo cha Echo vyema zaidi unamsaidia mgonjwa kupata huduma bora zaidi, kumpa taarifa sahihi itakayomsaidia katika matibabu yake pamoja na kujua tatizo lake kama linahitaji dawa ama upasuaji”, alisema Dkt. Delila

 
 

0 comments:

TAASISI YA MUSLIM WORLD LEAGUE INATEKELEZA MPANGO WA KWANZA WA UPASUAJI WA MOYO WA "LAPAROSCOPIC" NCHINI TANZANIA

Naibu Waziri wa Afya Nchini Malawi Mhe. Enock Phale akizungumza na wanahabari wakati wa ziara yake katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSS)

 Dar Es Salaam:

Taasisi ya Muslim World League itazindua mpango wa hali ya juu wa matibabu katika upasuaji wa moyo wa watu wazima katika Kituo cha Moyo JKCI katika mji mkuu wa Tanzania, Dar es Salaam, kuanzia tarehe 14 hadi 19 Agosti, kwa ushirikiano na Wizara ya Afya ya Tanzania na Kituo cha Upasuaji wa Moyo.

Hayo yamesemwa na Mkurugezi Taasisi ya Muslim World League Nchini Tanzania, Hassan Katungunya wakati wa ugeni wa Naibu Waziri wa Afya kutoka nchini Malawi Mhe. Enock Phale kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. 

Katika kutekeleza mpango huo teknolojia bora na za kisasa zaidi zitatumika na kwa mara ya kwanza nchini Tanzania, "roboti" maalumu katika upasuaji wa moyo itaanzishwa. Hii husaidia kupunguza kukaa kwa mgonjwa hospitalini, pamoja na kupunguza hatari ya kuambukizwa na kasi ya mgonjwa kurudi kwenye maisha ya kawaida ndani ya kipindi kifupi.

Mpango huu ni mpango maalumu wa kwanza kufanyika nchini Tanzania kwa kutumia vifaa vya hali ya juu na chini ya usimamizi wa timu ya madaktari bingwa na madaktari bingwa wa upasuaji inayoongozwa na Prof.  Othman Al-Uthman.

Timu ya upasuaji ya chama itafanya operesheni ngumu kwa kikundi cha wagonjwa waliochaguliwa kwa uangalifu, baada ya kufanya vipimo vingi ili kuhakikisha afya zao na hitaji lao la kufanyiwa upasuaji huu.


Miradi ya afya inawakilisha kipaumbele cha juu kwa Taasisi ya Muslim World League, kwani inatoa huduma kamili za afya kwa vikundi dhaifu na masikini kote ulimwenguni, pamoja na juhudi na rasilimali zake za kuinua ubora na ufanisi wa huduma za afya katika nchi nyingi, kwa kushirikiana na mamlaka rasmi zinazohusika ndani yao.


Taasisi ya Muslim World League pia inatekeleza programu adimu na zenye thamani ya juu za afya, kwani ilitekeleza mipango mingi kama hiyo, ambayo ya mwisho ilikuwa nchini Mauritania mwaka jana.

Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Molle akizungumza  wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Afya Nchini Malawi Mhe. Enock Phale katika Taasisi ya Moyo ya JKCI kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
  Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel pamoja na Naibu Waziri wa Afya Nchini Malawi Mhe. Enock Phale wakati wa ziara yake katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. wa pili kushoto ni Mkurugezi Taasisi ya Muslim World League Nchini Tanzania, Hassan Katungunya
  Naibu Waziri wa Afya Nchini Malawi Mhe. Enock Phale akimjulia hali mtoto aliyelazwa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo Herieth Mapunda wakati wa ziara yake katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.

0 comments:

NAIBU WAZIRI WA AFYA NCHINI MALAWI AFANYA ZIARA JKCI KUJIFUNZA UTOAJI HUDUMA ZA MATIBABU YA MOYO NCHINI

  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akielekeza huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo wakati wa ugeni wa Naibu Waziri wa Afya kutoka nchini Malawi Mhe. Enock Phale kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA).
  Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya akielezea huduma zinazotolewa katika chumba cha upasuaji mkubwa wa moyo kwa Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel pamoja na Naibu Waziri wa Afya Nchini Malawi Mhe. Enock Phale wakati wa ziara yake katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
  Naibu Waziri wa Afya Nchini Malawi Mhe. Enock Phale akimjulia hali mtoto aliyelazwa katika wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo Herieth Mapunda wakati wa ziara yake katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. 
  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimuonesha Naibu Waziri wa Afya Nchini Malawi Mhe. Enock huduma mbalimbali za Taasisi hiyo zinavyofanyika wakati wa ziara yake katika Taasisi hiyo kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. 
: Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Afya Nchini Malawi Mhe. Enock Phale wakati wa ziara yake katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kuangalia mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.

Na: Genofeva Matemu – JKCI

18/08/2022 Naibu Waziri wa Afya wa nchini Malawi ametembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa pamoja na kujifunza mifumo ya Tehama inayotumika katika uendeshaji wa huduma za matibabu katika Taasisi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Waziri wa Afya Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel alisema kuwa ugeni wa naibu waziri wa afya kutoka nchini Malawi umelenga kupata uelewa wa huduma zinazotolewa na JKCI pamoja na kujifunza mifumo ya Tehama ambayo Tanzania inaitumia kwenye sekta ya afya ili nao waende kuboresha mifumo ya afya nchini mwao.

Mhe. Mollel alisema kuwa uwekezaji mkubwa uliofanywa katika taaluma ya afya na vifaa tiba imeleta tija kubwa kwani sasa nchi za Afrika na nchi ambazo zinaizunguka Tanzania zimeanza kujifunza kupitia Tanzania na kuona badala ya kuwapeleka wagonjwa wao India, Ulaya na Marekani waanze kuwaleta hapa nchini.

 “Upande wa upasuaji mdogo wa moyo kupitia tundu dogo kwenye paja wataalamu wetu wameweza kufanya aina tofauti tofauti za upasuaji ambapo hadi sasa asilimia 92 ya upasuaji mdogo wa moyo unafanywa na wataalamu na asilimia nane iliyobaki inafanywa na wataalam kutoka nje ya Tanzania ambapo tunawachukua wataalam hao kuja hapa kwetu kwasababu vifaa tunavyo tunachotaka kutoka kwao ni ujuzi ambao utatuwezesha kwenda hatua ya juu zaidi”,

“Upasuaji mkubwa wa kufungua kifua asilimia 85 za upasuaji huo inafanywa na wataalam wa afya wazawa huku asilimia 15 za upasuaji huo inafanywa na wataalam wa afya kutoka nje ya nchi ambao wamekuwa wakituachia ujuzi kwa wataalamu wetu”, alisema Dkt. Mollel

Mhe. Dkt. Mollel alisema kuwa hivi sasa Taasisi ya Moyo inapokea wagonjwa kutoka nchi 25 duniani ikiwemo Visiwa vya Comoro, Zambia, Kenya, Congo, Malawi na nyinginezo hii inatokana na Uongozi wa Mhe. Rais Samia ambaye tokea Mwanzo alisema kuwa anaifungua nchi kwa maana ya kufungua fursa ya ujuzi, utalii wa kimatibabu na uduma za kibobezi za afya zinazopatikana hapa Tanzania.

Mhe. Dkt Mollel alisema kuwa Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania amewekeza kwenye eneo la afya ambapo Afrika hadi sasa zipo nchi chache ambazo zinafanya upasuaji wa moyo mbalimbali hivyo kuzivutia nchi ningine kama Malawi kuona ni vyema leo kuja kujifunza kwetu.

“Mhe. Naibu waziri wa Afya kutoka Nchini Malawi Mhe. Enock Phale amekuja hapa kwetu kwa ajili ya kuona huduma tunazizitoa na kujifunza mifumo ya Tehama tunayoitumia katika sekta ya afya hii inaonyesha adhma ya Mhe. Samia ya utalii wa kimatibabu inavyotekelezeka”,

Tukiwa wabunifu wakutosha kwa kuwatengenezea wataalamu wetu ujuzi na kuvisimamia vizuri vifaa vyetu tukapata wagonjwa wengi kutoka nje ya Tanzania mapato ya Taasisi zetu yataongezeka hivyo kuziwezesha Taasisi zetu kujiendesha zenyewe na kupunguza kuitegemea serikali”, alisema Dkt. Mollel

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi alisema kuwa ugeni wa Naibu Waziri wa Afya wa nchini Malawi umelenga kujifundisha JKCI inachokifanya na itawasaidiaje kama nchi na wao kuweza kufika Tanzania ilipo katika Sekta ya Afya.

“Malawi wanapita njia ambayo sisi tumepita huko nyuma ambapo wagonjwa wote wa moyo, figo, saratani, mifupa na magonjwa ya damu tulikua tunawapeleka India, Afrika ya Kusini, Ulaya na Marekani lakini baada ya uwekezaji huu mkubwa uliofanywa na Serikali JKCI imepunguza kupeleka wagonjwa wa moyo nje ya nchi kwa asilimia 95”,

“Katika hii miezi mitatu tumeshapata ugeni kutoka Afrika ya Mashariki, ugeni kutoka Zambia, na tukapata ugeni kutoka Mozambique, hii ni nchi ya nne sasa inakuja JKCI kwa ajili ya kuona nini tunafanya ili na wao wakafanye kama sisi”, alisema Prof. Janabi

Aidha Prof. Janabi alisema kuwa Serikali ina nia kubwa katika utalii tiba hivyo katika lile lengo la kufikisha watalii milioni 5 sekta ya afya chini ya usimamizi wa Wizara imekusudia afya ichangie katika kuleta watalii kupitia huduma bora na bobezi za matibabu yanayotolewa hapa nchini yakiwemo matibabu ya moyo.

“Tunaishukuru Serikali kwa ushirikiano waliotupatia kwa kuwekeza wataalamu na vifaa tiba vya kisasa katika Taasisi yetu, sisi kama wataalam kazi yetu ni moja tu ya kuwahudumia wananchi wa Tanzania na nchi za jirani za SADC ikiwemo kutangaza utalii kupitia afya”, alisema Prof. Janabi

Naye Naibu waziri wa afya Nchini Malawi Mhe. Enock Phale alisema kuwa amekuja Tanzania kwa ajili ya kujifunza Tanzania imewezaje kufanikiwa katika kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo na kuangalia namna ambavyo nchi yake itaweza kuwaleta wagonjwa wa moyo badala ya kuwapeleka nchi za India na Ulaya.

“Natamani na sisi Malawi tuwe kituo cha ubora katika kutoa huduma za matibabu ya moyo kwani sasa tunatumia fedha nyingi kuwapeleka wagonjwa wetu nchini India kwa ajili ya matibabu ya moyo wakati majirani zetu hapa mmefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kutoa huduma za matibabu ya moyo”,

“Naamini kwa kuwaleta wagonjwa hapa Tanzania kutapunguza gharama za matibabu, Malawi ni nchi wanachama wa SADC hivyo kupitia mwavuli huo tunaenda kufanikiwa kwa wagonjwa wetu kuja kutibiwa hapa JKCI”, alisema Mhe. Phale

                                                                             

0 comments: