RAIS PUTIN: MACHAFUKO ENEO LA MASHARIKI YA KATI YANASABABISHWA NA KUPENDA KUJITANUA KWA BAADHI YA PANDE

Rais Putin: Machafuko eneo la Mashariki ya Kati yanasababishwa na kupenda kujitanua kwa baadhi ya pande.
Rais Vladmir Putin wa Russia amesema kuwa, hali ya sasa ya eneo la Mashariki ya Kati imekuwa mbaya kutokana na njama za baadhi ya madola katika kulisukuma eneo hilo kuelekea kwenye maslahi yao binafsi.
Rais Putin aliyasema hayo Alkhamisi ya jana na kuongeza kuwa, baadhi ya madola yanafanya njama kupitia mapinduzi ya kijeshi na nguvu za kijeshi, kwa lengo la kuyaelekeza matukio ya eneo la Mashariki ya Kati kwenda upande wa maslahi yao binafsi. Amefafanua kuwa, hadi sasa baadhi ya nchi badala ya kupambana na ugaidi, zinajaribu kuvuruga usalama na amani ya eneo hilo. Rais Vladmir Putin ameongeza kuwa, katika uwanja huo Russia kwa kushirikiana na serikali halali ya Syria na baadhi ya nchi za eneo, zinapambana na magaidi kwa kufuata sheria za kimataifa.

Uhasama uliopo kati ya Marekani na Russia
Aidha Rais Putin ameashiria mgogoro wa eneo la Peninsula ya Korea na kusema kuwa, ni lazima mgogoro huo kutatuliwa kwa njia za amani. Akieleza kuwa, baadhi ya nchi zinatekeleza njama kupitia njia za kisiasa kwa ajili ya kudhamini maslahi yao ya kiuchumi, amesema kuwa, baadhi ya hatua za kisiasa zina malengo ya kibiashara na kwamba lengo la vikwazo vilivyopitishwa hivi karibuni na kongresi ya Marekani dhidi ya Russia, ni kuiondoa Moscow katika soko la nishati barani Ulaya.

0 comments: