MAGAZETI YA LEO NOVEMBAR 01, 2016

0 comments:

SABABU ZA KUANGUKA NDEGE YA BRAZIL ZATAJWA

Colombia
Visanduku vya mawasiliano ajali ya ndege ya Brazil vyapatikana
Ndege iliyokuwa imewabeba wachezaji wa timu ya mpira kutoka nchini Brazil ambayo ilipata ajali nchini Colombia inasemekana kwa muujibu wa taarifa zilizovuja ndege hiyo iliishiwa mafuta kutoka katika kifaa cha kurekodia mawasiliano.
Katika mnara wa mawasiliano ya ndege , rubani alisikika akirudia mara kadhaa akiomba ruhusa ya kutua kwa dharura kutokana na hitilafu ya umeme iliyokuwamo ndegeni pamoja na kuishiwa mafuta ya ndege.
Kabla hata mawasiliano hayo yaliyorekodiwa kufikia mwisho ,rubani alisikika akisema yuko angani umbali wa futi elfu tisa sawa na mita elfu mbili mia saba na arobaini na tatu.Taarifa za mawasiliano hayo zimekuwa gumzo katika mitandao kadhaa nchini Colombia na hata katika vyombo vya habari nchini humo, na hivyo kumekuwepo fununu za taarifa hizo kuwa huenda zikawa na chembe ya ukweli kwamba kuishiwa kwa mafuta ndiyo chanzo zha ajali ya ndege hiyo.
Wanajeshi wa Colombia waliliambia shirika la habari la AFP, kwamba pamoja na ndege hiyo kuanguka kuna shaka juu ya ajali hiyo kwani pamoja na ndege hiyo kuanguka hakukuwa na mlipuko wowote na kwamba huenda kulitumika nguvu ingine tofauti na nadharia ya kwisha kwa mafuta ndegeni.
Wadadisi wa mambo na wachunguzi bado hawako tayari kufungua mdomo na kuzungumzia juu ya chanzo chochote cha ajali hiyo na kwamba taarifa kamili ya uchunguzi itatolewa baada ya miezi kadhaa.
Wachezaji wa timu ya Chapecoense walikuwa safarini kuelekea nchini Colombian kwenye mji wa Medellin mahali kulikotarajiwa mechi kubwa ya mpira wa miguu ya kihistoria na badala yake wachezaji hao wameacha historia .Kufuatia vifo vya wachezaji wa timu hiyo, ulimwengu mzima umeungana kuomboleza vifo vyao.
Kwa muujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka katika shirika la ndege la Lamia watu wanne waliokuwa wasafiri na ndege hiyo wameponea chupuchupu kuwa miongoni mwa waliokufa baada ya kukosa tiketi.
Mmoja wa manusura wa ajali hiyo ambaye ni fundi wa ndege Erwin Tumiri, ameeleza namna alivyokwepa kifo, kwamba yeye alifuata maelekezo yote ya namna ya kujiokoa ,anasema abiria wenzie , walio wengi walisimama na kuanza kupiga kelele nay eye aliamua kuweka sanduku lake la kusafiria kati kati ya miguu yake na kuamua kubaki hivyo.
Visanduku viwili vya mawasiliano vya ndege hiyo vyote vilipatikana na tayari vimeanza kufanyiwa uchunguzi na wataalamu wa masuala ya anga.
Wachunguzi wataalamu kutoka nchini Uingereza wanasaidiana na mamlaka za Amerika Kusini kwasababu ndege iliyopata ajali ilitengenezwa na wana anga wa Uingereza BAE nchini Uingereza.Brazil imeanza siku tatu za maombolezo wakati maelfu ya watu na washabiki wa timu ya Chapecoense wako katika mji yaliko makao makuu ya timu hiyo Chapeco wanaendelea mkesha wa maombolezo wakati maandalizi ya kuchukua mabaki ya wachezaji hao inafanywa na jeshi kurejeshwa Brazil ili kuzikwa kwa pamoja katika uwanja wa Chapeco.
Nchi ya Bolivia tayari imekwisha tuma ndege ya kuchukua mabaki ya raia wake waliokufa katika ajali hiyo nchini Colombia.
Timu hiyo iliandika historia ya mafanikio katika soka kwa kuwa kileleni mwa ligi ya Brazil kwamara ya kwanza mwaka 2014.Kati ya watu 77 waliokuwa wameabiri ndege hiyo miongoni mwao ni watu sita tu ndiyo walionusurika .Abiria walio wengi walikuwa ni wachezaji wa timu ya Chapecoense na waandishi habari wapatao ishirini walikuwa miongoni mwa walipoteza maisha .BBC

0 comments:

MAJIVU YA FIDEL CASTRO KUSAFIRISHWA SANTIAGO

Kuba Trauer um Fidel Castro (Reuters/E. De La Osa)
Mji wa Santiago unaojulikana kama chimbuko la ukomunisti wa Cuba, ndiko mapinduzi yaliyoongozwa na marehemu Castro yalianzia mnamo mwaka 1953 na akachukua urais mwaka 1959.
Baada ya mamia ya maelfu ya watu kuhudhuria misa ya wafu kwa mwanamapinduzi wa Cuba Fidel Castro, majivu ya marehemu huyo yanaanza kusafirishwa leo kutoka jiji kuu Havana hadi Santiago kufanyiwa mazishi hapo siku ya Jumapili. Huo ukiwa umbali wa kilomita 900. Maelfu kwa maelfu ya wacuba wanatarajiwa kuwa barabarani kushuhudia majivu hayo yatakapokuwa yakisafirishwa. 
Mwili wa Fidel Castro aliyefariki akiwa na umri wa miaka 90, Ijumaa wiki jana, ulichomwa moto kulingana na matakwa yake. Majivu yake yatapitishwa katika miji kadhaa nchini humo kwa siku tatu kwanzia leo, kabla ya kufikishwa mji wa Santiago ambako ndiko atazikwa siku ya Jumapili.
Mji wa Santiago unaojulikana kama chimbuko la ukomunisti wa Cuba, ndiko mapinduzi yaliyoongozwa na marehemu Castro yalianzia mnamo mwaka 1953 na akachukua urais mwaka 1959.  Hapo jana mamia ya maelfu ya waombolezaji walifika kumpa heshima za mwisho jijini Havana. 
Rais wa Bolivia ni miongoni mwa waliohudhuria misa hiyo na alisema: "Fidel hajafa kwa sababu wanaopigania uhuru hawafariki. Huyo ni Fidel. Hajafa kwa kuwa mawazo hayafi hasa mawazo yanayoleta ukombozi. Fidel hajafa kwa kuwa mapigano hayajaisha hasa mapigano dhidi ya utengano. Fidel ni kama yuko hai kuliko zamani akiendeleza vita kuokoa makazi yetu ya pamoja".
Mazishi yake yanatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kimataifa wakiwemo marais Nicolas Maduro wa Venezuela, Daniel Ortega wa Nicaragua, Evo Morales wa Bolivia na Rafael Correa wa Equador, kando na wakuu wa nchi za Amerika ya kusini na mfalme wa zamani wa Uhispania Juan Carlos.
Uhusiano wa Cuba na Marekani
Fidel Castro alitawala Cuba kwa miaka 47, hadi alipojiuzulu mwaka 2006 kufuatia hali yake ya kiafya, na kumkabidhi nduguye Raul Castro. Tangu wakati huo hajajitokeza hadharani japo inaaminika alikuwa na wasiwasi na uhusiano ulioimarishwa mwaka 2014 kati ya nchi yake na hasimu wao wa jadi Marekani. Haijabainika ikiwa uhusiano huo utaendelea kuimarika baada ya Januari rais mteule wa Marekani Donald Trump atakapochukua rasmi urais.
Akitoa hotuba ya rambirambi jijini Havana, rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesema "Cuba haikutafuta madini ya dhahabu, almasi au mafuta barani Afrika. Wacuba walitaka uhuru na mwisho wa unyanyasaji wa bara la Afrika kutumiwa kama kiwanja cha kuchezewa na nchi kubwakubwa huku watu wakiteseka".
Fidel Castro alipendwa na wengi duniani hasa Amerika ya kusini na Afrika, kwa kusimama dhidi ya Marekani, huku akizindua mipango ya elimu bure na huduma za afya bila malipo kando na kuwatuma madakitari wao katika mataifa mengine duniani kutoa misaada ya kiafya.
Lakini wengine walimshutumu kuwa kiongozi wa kiimla aliyevuruga uchumi kutokana na sera zake za usosholisti na kuwanyima wacuba haki za kibinadamu mfano uhuru wa kujieleza.DW

0 comments:

UNESCO-TANZANIA YAWAJENGEA UWEZO MAAFISA KUTOKAWIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO KATIKA KUTEKELEZA MPANGO MKAKATI WA WIZARA MAWAKA 2016/2017

 Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO), nchini Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigueas, (kulia), akiendesah semina ya mafunzo ya siku tatu kujenga uwezo kwa maafisa wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, makao makuu ya UNESCO, Oysterbay jijini Dares Salaam, jana Novemba 30, 2016. Kushoto ni Mwanasheria wa Wizara, Bw.Evordy Kyando.

NA K-VISBLOG/KHALFAN SAID
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni , (UNESCO), limeendesha mafunzo ya siku tatu kwa maafisa wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ili kuwajengea uwezo wa kutekeelza mpango mkakati wa wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Mafunzo hayo yaliyoanza leo Novemba 30, 2016, na kuendeshwa na Mkuu wa Ofisi ya UNESCO, nchini, Bi. Zulmira Rodrigues yanafanyika kwenye ofisi za shirika hilo, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
“Tumekusanyika hapa kwa mara ya kwanza kuisaidia wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ili kuboresha uwezo wawafanyakazi wake, wafanyakzi kutoka idara tofauti tunao hapa, wapo kutoka idara ya Habari, Utamaduni, michezo pamoja na idara za kiusaidizi kama vile fedha, sheria, ICT na kadhalika.” Alianza kwa kusema Mkuu huyo wa UNESCO.
Alisema, Mpango unaweza kusaidia kufanya tathmini na marekebisho kwa mahitaji ya wizara au taasisi yoyote ile na kwa kuzingatia hilo, Shirika hilo limeona upo umuhimowa kuwajengea uwezowatendaji katika wizara hiyo ili kutekeleza vema mpango mkakati wa wizara. “Kama huna mpango wowote ule uliouweka, utajikuta unatumia nguvu nyingi na kuishia patupu bila mafanikio yoyote yale.” Alisema.
Alisema, wafanyakazi katika taasisi yoyote ile ni wajibu kushirikiana ili kuwa na lengo moja kufikia malengo mahsusi yaliyopangwa na Wizara au taasisi. “Kabla ya kuweka mpango wowote ni lazima kufanyike utafiti wa hali halisi ya jambo linalotaka kushughulikiwa.” Alifafanua Bi. Zulmira.
Washiriki walianza kujifunza mambo mbalimbali ama vile, namna ya kutambua tatizo la msingi, uwezo, udhaifu, fursa na tishio mambo yote hayo yanayojulikana kitaalamu kama (SWOT Analysis), ndiyo yatakayotoa picha halisi ya namna ya kupanga mkakati na namna ya kuutekeleza mkakati huo.



Aidha washiriki wa warsha hiyo wamefurashiswa na mafunzo hayo kwani yatasaidia kuwajengea uwezo wa kutekeelza kikamilifu malengo ya kiofisi na binafsi.
“Mafunzo haya yatanisaidia sana katika kutekeleza malengo yaliyopangwa kwani nimejifunza njia mbalimbali za kimkakati katika kutekeleza malengo yaliyopo.” Amesema mshiriki Lorietha Lawrence, afisa habariwizara ya Habari, Utamaduni, Sanaana Michezo.
Kupitia mafunzo haya, ninahakika yatasaidia kutekelza majukumu yangu ya kila siku, na nitakachojifunza nitashirikiana na wenzangu kwenye kitengo chetu katika kutekelezaipasavyo majukumu yetu.” Alisema Afisa mwingine wa habari, Lilian.

 Baadhi ya washiriki
Mshiriki kutoka idara ya utamaduni, Sefania Molela, akizungumza
 Mshiriki kutoka idara ya Habari akizungumza
 Bi. Zumlira Rodrigues, (kulia), akiteta jambo na Afisa Mpango wa Utamaduni wa UNESCO, Rahma Sudi
 Afisa Mpango wa UNESCO, Michaela Konopikova
 Mtaalamu wa masuala ya ICT wa UNESCO, Leonard Kisenha, (katikati), na Afisa Mpango, Utamaduni wa Shirika hilo, Michaela, (kushoto0, wakitazama kitu kwenye kompyuta
 Mkufunzi wa UNESCO, Deirdre Prins-Solan
 Mshiriki kutoka idara ya utamaduni, akizungumza

 Mshiriki kutoka idara ya Michezo akizungumza
 Bi.Zulmira akiendesha mafunzo
 Maafisa mpango-Utamaduni wa UNESCO, Rehema (kulia) na Michaela wakijadiliana jambo muda mfupi kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo
 Bi.Zulmira akiendesha mafunzo
Mwanasheria wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Evordy Kyando, akizungumza jambo
Khalfan Said Chief Photographer/Owner K-VIS MEDIA P.Box 77807 Mobile; +255 646-453/+255-653-813-033 Office; Mivinjeni Opp.Tanesco, Kilwa RD Blog:http//khalfansaid.blogspot.com Dar es Salaam, Tanzania

0 comments:

MUUZA MITUMBA SOKO LA KARUME JIJINI DAR ES SALAAM AFUTIWA LESENI YA BIASHARA KWA KUMDHALILISHA MTEJA WAKE WA KIKE



 Diwani wa kata ya Mchikichini, Joseph Ngowa (katikati), akihutubia wakati akizindua kampeni ya siku 16 ya kupinga ukatili wa kijinsia iliyoandaliwa na Shirika la Eguality for Growth (EfG), Dar es Salaam jana asubuhi.Kushoto ni Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Wanawake katika Soko la Mchikichini, Betty Mtewele na kulia ni Ofisa Mtendaji wa Kata ya Mchikichini, Charles Kapongo.
read more

0 comments:

WATUMISHI OFISI YA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA WAPIGWA MSASA

 
Mshauri Mwelekezi wa Masuala ya Jinsia kutoka “Women Fund” Profesa Ruth Meena akitoa mada.

 Mshauri Mwelekezi wa Masuala ya Jinsia kutoka “Women Fund” Profesa Ruth Meena (kulia), akiwasilisha mada juu ya jinsi ya kuingiza masuala ya jinsia katika mpango kazi wa taasisi wakati wa kikao kazi cha watumishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kilicho fanyika jana katika Ukumbi wa ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam.
 Mafunzo yakitolewa.

0 comments:

RAIS LUNGU WA ZAMBIA AONDOKA NCHINI

Rais John Magufuli akiagana na Rais wa Zambia, Edgar Chagwa Lungu kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere wakati mgeni huyo alipoondoka nchini kurejea nyumbani jana Novemba 29, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
  Rais John Magufuli akiwapungia wananchi waliojitokeza kumuaga Rais wa Zambia, Edgar Chagwa Lungu kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere wakati alipoondoka nchini kurejea nchini Novemba 29, 2016. Wengine pichani ni Makamu wa Rais, Samia Suluhu na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Inspekta Jenerali wa Polisi, Ernest Mangu kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Novemba 29, 2016. Wapili kulia ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange na watatu kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi John Kijazi.
 Rais John Magufuli akiongozana na  mgeni wake, Rais Edgar Chagwa Lungu wakati mgeni huyo alipoondoka nchini kurejea nyumbani kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es salaam Novemba 29, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Rais John Magufuli na Makamu wa Rais, Samia Suluhu wakishuudia wakati Rais wa Zambia Edgar Chagwa Lungu akiagana na Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa kwenye uwanja wa ndege wa Julius Kambarage Nyerere kabla ya kuondoka nchini kurejea nyumbani Novemba 29, 2016.

0 comments: