RAIS SAMIA LEO AHITIMISHA TAMASHA LA KIZIMKAZI 2026

 

Kusini Unguja, Zanzibar 

Leo nimehitimisha Tamasha la Kizimkazi 2026, baada ya siku tatu za shangwe, fursa na shughuli mbalimbali zilizolenga kujenga umoja, kukuza fursa za biashara na uwekezaji, kutangaza utamaduni na utalii wetu, pamoja na kufungua miradi ya maendeleo kwa wananchi. Tunatarajia matokeo ya shughuli hizi kuendelea kuonekana hata baada ya tamasha kumalizika.

Ninawashukuru wote walioshiriki na kufanikisha tamasha hili. Ninawasihi tuendelee kushikamana, tudumishe amani, utulivu na usalama wa nchi yetu, kwa kuwa ndiyo msingi wa maendeleo na ustawi wetu.



0 comments: