IRAN IKO TAYARI KUSHIRIKIANA NA SIERRA LEONE KATIKA KUPAMBANA NA UGAIDI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:19 AM
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria
mashambulio ya kigaidi katika baadhi ya nchi za Ulaya na Afrika na
kutangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kushirikiana na Sierra
Leone katika kupambana na ugaidi na misimamo ya kufurutu mpaka.
Muhammad Javad Zarif ametangaza msimamo huo hapa mjini
Tehran katika mazungumzo na Mohamed Gibril Sesay, Waziri wa Nchi Katika
Wizara ya Mambo ya Nje ya Sierra Leone aliyeko safarini hapa nchini.
Katika mazungumzo hayo Dakta Zarif amesema, kwa upande wa kisiasa,
kiuchumi na kiutamaduni, bara la Afrika lina umuhimu maalumu kwa Jamhuri
ya Kiislamu ya Iran; na kustawisha uhusiano na nchi za bara hilo
kumekuwa kukipewa kipaumbele na Iran tangu baada ya Mapinduzi ya
Kiislamu.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria pia uwezo na fursa za
kiuchumi zilizopo katika uhusiano wa Iran na Sierra Leone na kueleza
kuwa katika kipindi kipya cha uongozi wa Rais Hassan Rouhani, nchi hizi
mbili zinaweza kustawisha zaidi uhusiano wao wa kiuchumi kwa kutumia
mikakati ya kivitendo.
Kwa upande wake, Mohamed Gibril Sesay, Waziri wa Nchi Katika Wizara
ya Mambo ya Nje ya Sierra Leone amesisitizia umuhimu wa uhusiano wa nchi
yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kueleza kwamba kustawisha
uhusiano katika nyanja zote ni jambo linalopewa kipaumbele na nchi yake.
Aidha ametilia mkazo nafasi na mchango muhimu wa Iran katika kuleta
amani na uthabiti katika eneo la Mashariki ya Kati na mapambano dhidi ya
ugaidi na kubainisha kuwa Sierra Leone iko tayari kushirikiana na Iran
katika kupambana na ugaidi na misimamo ya kufurutu mpaka.../
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: