MADIWANI WALIA NA UHALIBIFU WA MAZINGIRA MKOANI KIGOMA



NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA

BARAZA la Madiwani wilaya ya Kakonko mkoani kigoma wamesikitishwa na kitendo cha uharibifu wa mazingira unaofanywa na wakimbizi waishio katika Kambi ya Mtendeli iliyopo humo,huku ofisi za idara ya wakimbizi na stahiki za malipo wakizielekeza wilaya ya kibondo,ambapo ni kinyume cha sheria husika.
                                                    
Hayo yalibainikamwishoni mwa wiki  katika kikao cha Baraza hilo  katika kipindi cha maswali na majibu katika kutatua kero za umma kupitia idara mbalimbali  baraza hilo lilihitaji majibu sahihi kutoka kwa mkuu wa kambi kigoma sababu ya kuweka ofisi kibondo na kulipa stahiki wakati uharibifu wa mazingira unafanywa wilaya ya kakonko.

Awali Diwani Steven Mnigankoko alisema changamoto ya ukataji miti holela umekithiri wilayani humo,huku stahiki za kuhifadhi wakimbizi zikielekezwa wilaya ya kibondo hali kadhalika ofisi za idara hiyo ipo huko ilihali janga la ukataji miti unafanyika kakonko na kwa mujibu wa sheria stahiki na ofisi ziwepo eneo linalohifadhi wakimbizi na si vinginevyo.

Akiongezea hilo Mbunge wa Jimbo la Buyungu Kasuku Bilago alisema kisheria walihitajika kuweka ofisi na stahiki katika eneo linalohifadhi wakimbizi kwa kutoa huduma za kijamii katika maeneo yanayoathirika na uwepo wao ambapo miti mingi inatumika hovyo hali inayotishia mabadiliko ya tabia nchi,kwa kuwa hakuna jitihada za makusudi kupunguza uharibifu huo.

Akijibia hilo Mkuu wa Kambi ya wakimbizi Mtendeli Innocent Mwaka alisema changamoto hiyo inatokana na historia ya wilaya ya kibondo ambayo ilibeba kambi zaidi ya mbili na kugawanywa kwa wilaya hizo ni chachu ya ofisi kubaki humo na stahiki kwa ujumla.

Akiongezea hoja hiyo   Mwenyekiti wa halmashauri ya kakonko Juma Maganga alisema changamoto hiyo inajulikana na waziri mwenye dhamana na linafanyiwa kazi na katibu wa wizara ya mambo ya ndani hivyo hawana budi kuliacha kama lilivyo hadi hapo taratibu za serikali kuu itakapotoa tamko rasmi.
Mwisho.

0 comments: