KAYA 307 ZAGUNDULIKA HAZINA VIGEZO MRADI WA TASAF BUHIGWE MKOANI KIGOMA

NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA

Mkuu wa wilaya ya Buhigwe Mkoa wa Kigoma Kanal Marko Gaguti amethibitisha kuwepo kwa kaya 307 katika wilaya hiyo, zilidanganya tarifa zao hatimaye  kunufaika na mradi wa Mfuko wa kusaidia kaya maskini sana, TASAF wakati  hazina sifa na vigezo wa kunufaika na mfuko huo.
Akitoa kauli hiyo katika ziara ya siku 10 ya kukagua kaya zilizokuwa katika mpango wa kupunguza umaskini kwa walengwa wa TASAF Gaguti alisema kwa Tasaf awamu ya tatu wasio na sifa wataondolewa kwa kuwa hawana vigezo hali iliyochangia wananchi wengi waliongia kwa hila kukimbia kaya zao na katika hili wamejiondoa wenyewe.
“ziara hii ya nyumba kwa nyumba inashirikisha viongozi kuanzia ngazi ya kijiji, kata na wilaya ili kubaini uhalisia wa maisha ya sifa ya walengwa wa mfuko wa TASAF , kubaini maisha yao na waliodanganya wataondolewa na kuingizwa wenye sifa, serikali ina dhati ya kupunguza umaskini, viongozi shirikianeni na serikali yenu” alifafanua Kanal Gaguti.
Kwa upande wa Mratibu wa TASAF wilaya ya Buhigwe, Chubwa Deogratius alisema katika ziara ya juzi walibaini kaya mbili katika kata ya Mnanila hazina vigezo vya kupata fedha katika mfuko huo ambao ni Anjelina Josia na Veronika James hawana sifa na vigezo vya kutumia fursa hiyo na wanaendelea kupita nyumba hadi nyumba kwa wanufaika wote wa awamu ya tatu ili kujiridhisha na tarifa za awali zilizowaingiza katika mpango huo.
Akisisitiza hilo Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali Mstaafu, Emanuel Maganga alisema kwa yeyote aliyewahi kuingizwa katika mpango wa TASAF na hana vigezo na sifa za kuwa miongoni mwa wanufaika watafikishwa katika vyombo vya sheria na watalipa fedha zote walizowahi kulipwa na mfuko huo, kwa kuwa ndio chanzo cha kikwazo cha maendeleo kwa walengwa wa mfuko huo.
Maganga aliongeza kuwa, wananchi waliopokwa haki za kuingizwa katika mfuko huo wasubiri mwakani pindi utakapoisha ukomo wao na walengwa wataingizwa ili wahujumu wa hilo watapatiwa haki zao kwa mujibu wa sheria za nchi na kuomba wawe wavumilivu zaidi ili kuwapa fundisho wananchi wenye tabia ya uongo na ktumia rushwa ili wapate haki za wenzao.
Mwisho.

0 comments: