JESHI LA SYRIA LAENDELEZA MASHAMBULIZI DHIDI YA MAGAIDI HUKO HALAB

Duru za Syria zimearifu kuwa jeshi la nchi hiyo limeendelea kuwashambulia magaidi ili kuukomboa kikamilifu mji wa kihistoria wa Halab yaani Aleppo.
Duru za kijeshi za Syria zimeripoti kuwa wanajeshi wa nchi hiyo leo wamefanya mashambulizi ya nchi kavu na anga na kuendelea kusonga mbele huko mashariki mwa mji wa Halab ili kuwafurusha kikamilifu magaidi katika mji huo. Kituo cha Usuluhishi cha Russia kimeripoti kuwa raia zaidi ya elfu kumi wakiwemo watoto elfu nne wameondoka katika maeneo yanayoshikiliwa na magaidi huko Aleppo katika muda wa saa 24 zilizopita. 
Raia wa Syria wakiondoka huko Aleppo
Umoja wa Mataifa pia umetangaza kuwa magaidi wanawazuia raia kuondoka mashariki mwa mji wa Aleppo. Umoja huo umeeleza kuwa raia laki moja wa Syria wamezingirwa na magaidi mashariki mwa Aleppo.

0 comments: