GUNIA LA MKAA KUUZWA 50,000 KOANI KIGOMA




NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA

KUTOKANA na kupanda kwa ushuru wa bidhaa ya mkaa ,chama cha wauza mkaa mkoani kigoma wameadhimia kuuza gunia moja lenye ujazo wa kilo 50 kwa kiasi cha sh.50,000 ifikapo Desemba mosi mwaka huu.

Akifafanua hilo mbele ya gazeti hili Mwenyekiti wa chama hicho Fadhili Kiswaga alisema serikali ya awamu ya tano si serikali ya kufanya biashara kwa ujanjaujanja badala yake wadau wa mali asili hasa misitu hawana budi kufanya biashara kwa mujibu wa sheria na taratibu za wizara husika.

Kiswaga alisema, kupanda kwa gharama hiyo inachangiwa na gharama za ushuru wa serikali kuu ambapo hutozwa fedha sh.240 kwa kilo moja,serikali ya wilaya ambayo wanalangua mkaa wanatozwa sh.16,600 kwa kila gunia,kibali cha usafirishaji (TP)sh,7,500 sanjari na  Sh.1,000 kwa ajili ya upandaji miti.

“tunalangua kwa wakulima gunia moja kwa sh.12,000 ,jumla ya gharama ni  sh.47,100 hali inayotulazimu kuuza kwa jumla kwa bei hiyo kwa walaji wa nyumbani na kwa wateja wanaouz mitaani watalangua kwa sh.55,000 ili kila mtu achangie pato la taifa na si kukwepa sheria ambayo inanufaisha wachache” alibainisha Kiswaga.

Alisema awali walikuwa wakiuza gunia moja kwa sh.25,000 lakini katika usafirishaji wa zao hilo kuna shubiri na tamu ili kufikisha bidhaa kwa walaji,hali iliyopeleka chama kujipanga na kuratavyowakabili ili kufanya biashara kwa uwazi ili kuziba mianya ya rushwa ,huku akikiri serikali ya sasa ni  sheria bila shuruti.
Aliomba serikali isaidie kupunguza gharama za zao hilo kwa kuweka risiti katika vituo vya maliasili vilivyopo katika eneo la mizani  simbo ili kuepuka urasimu wa kupata risiti za ulipiaji wa zao hilo,ambapo kwa sasa wanalazimika kwenda halmashauri ya lugufu kulipia ilihali kuna uwezekano wa kuondoa usumbufu huo.
Mwisho.

0 comments: