Thursday, November 24, 2016

WAZUWWAR ZAIDI YA 80 WAUAWA SHAHIDI KATIKA SHAMBULIO LA KIGAIDI NCHINI IRAQ

Wafanyaziara (mazuwwar) zaidi ya 80 wamekufa shahidi leo kufuatia shambulio la kigaidi la bomu la kutegwa garini lililowalenga katika mji wa Hillah kusini mwa Iraq.
Taarifa za awali zinasema kuwa, wengi wa waliouawa shahidi katika shambulio hilo la kigaidi ni wafanyaziara wa Kiirani. Vyombo vya usalama vya Iraq vimetangaza kuwa, mlipuko huo wa bomu la kutegwa garini ulitokea katika kituo kimoja cha kujazia mafuta (petrol station) katika mji wa Hilla na kwamba, Mazuwwar hao waliokwenda nchini Iraq kwa ajili ya ziara ya Imam Hussein as walikuwa njiani kurejea makwao.
Mlipuko uliowalenga Mazuwwar wa Imam Hussein as Iraq
Bahram Qassemi, Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kulaani shambulio hilo la kigaidi ametangaza kuungana pamoja na familia za Wairanmi waliopoteza ndugu zao katika shambulio hilo la kigaidi. Amesema, jinai hiyo ni radiamali ya kushindwa mfululizo magaidi hao huko Iraq.
Bahram Qassemi amebainisha kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya iran itaendelea kuwa kando ya taifa la Iraq katika kupambana na ugaidi.

No comments:

Post a Comment