DC- KANALI NDAGALA AGIZA JESHI LA POLISI KUWAONDOA WALIOJENGA ZIZI LA MIFUGO KATIKA KITUO CHA AFYA- KAKONKO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 8:54 AM
MAGRETH
MAGOSSO,KIGOMA
MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala ameliagiza
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Serikali ya Kata ya Gwanumpu kuwaondoa
mara moja wafugaji waliovamia na kujenga zizi la Ng’ombe karibu na chanzo cha
maji na huduma za kijamii ilihali wanajua ni kunyume cha taratibu na sheria
husika
Akithibitisha
kauli hiyo juzi wilaya ya Kakonko alipotembelea baadhi ya vijiji vya wilaya
hiyo ambapo awali alipata malalamiko kutoka kwa wananchi kuwa kuna changamoto ya kuingiliana maeneo ya mashamba na baadhi ya wafugaji
kukiuka sheria za mamlaka kwa kujenga zizi la mifugo katika kituo cha
afya,shule na chanzo cha maji ni kero kwa serikali, hali inayoashiria kutokea
matukio ya mauwaji huku akizitaka mamlaka husika kuweka matumiza bora ya adhi sanjari
na wananchi wafuate taratibu na sheria zilizowekwa.
‘’kero
hii huanza taratibu yapoachwa uongezeka mwishowe kusababisha madhara
makubwa na kupelekea watu kuuwana kisa mgogoro wa ardhi kwa ajili ya malisho na
kilimo hivyo ,isipodhibitiwa vifo na upotevu
wa rasilimali nuvu kazi ya Taifa ‘’alisema Kanali Ndagala
James
Myelekano, ni mmoja wakazi wa Kijiji cha Bukiliro, Kata ya Gwanumpu
chenye wafugaji wengi alisema kuwa viongozi wa vijiji watenge
maeneo yanayoeleweka kwa jamii hizo,na sheria,taratibu
ziwe wazi ,ili kuepusha majanga, nakuiomba serikali iwaondoe haraka waliovamia maeneo ya mashamba kwa ajili
ya mifugo .
Kwa
niaba ya wakulima Deogratias Kavano alifafanua
kuwa, kuna mfugaji mmoja amehamishia mifugo yake katika eneo la vyanzo vya maji
na kuchunga mifugo yake katika sehemu zinazotolewa huduma za afya na shule na
kukataa kutoa mifugo yake .
Akithibitisha
hilo Mwenyekiti wa kijiji cha Gwanumpu Festo Sulila akiri Mfugaji huyo kujenga Zizi la Ng’ombe jirani na Kituo cha
Afya cha Gwanumpu na Shule ya sekondari ya Gwanumpu licha ya kutostaili kuwepo kwa zizi hilo katika
eneo hilo la makazi ambapo inawapa kero ya harufu mbaya lakini anakataa kutoka
hapo.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: