Waraghbishi toka vijiji vya Iponya, Nyakasumula, Bukandwe na Shenda wakiwa katika picha
ya pamoja na mwenyekiti na mtendaji wa kijiji cha Shenda.
……………………………………………………………………………
Ni miaka mitatu na miezi nane
toka mraghbishi Fedson Yaida na wenzake toka vijiji vya jirani kukutana na
Chukua Hatua. Ni rafiki waliyekutana naye mwaka 2011 katika mazungumzo maalumu
ambayo walitakiwa kuyafikisha kwa wananchi wenzao wa vijiji vya Shenda, Iponya,
Nyakasumula na Bukandwe katika wilaya ya Mbogwe mkoani Geita. Ni katika mazungumzo hayo ya siku tatu,
ambayo Fedson toka kijiji cha Shenda alibadilishwa na kuwa mraghbishi wa
aling’amua uwezo alio nao katika kusimamia rasilimali za kijiji chao, suala ni angezisimamiaje
wakati yeye si kiongozi na ni jukumu la wanakijiji
wote. Katika mazungumzo hayo rafiki yao, Chukua Hatua aliwaambia, “Ni jukumu lako
Fedson na waraghbishi wengine mliopo hapa, ni jukumu lenu la msingi kuj i t aj
i r i sha kwa taarifa na maarifa. Kwa kufanya hivyo mtakuwa na uwezo wa kujenga
hoja mkizithibithisha na vielelezo. Hivyo ni jukumu lenu kujua ni wapi na toka
kwa nani mtapata taarifa na vielelezo vya hoja yenu. Uzito wa hoja na maelezo
kwa uthibitisho ni silaha muhimu kama mnataka kushawishi wenz e n u k u c h u k u a hatua.” Baada ya maelezo hayo walitakiwa kwenda
kutembelea halmashauri ya wilaya yao, wakati huo ikiitwa Bukombe. Na baadhi ya maeneo
hayo ni ofisi za Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri. Maelezo haya yalilenga
katika haki ya kupata taarifa, kwa mujibu wa ibara ya 18 ya Katiba.
toka mraghbishi Fedson Yaida na wenzake toka vijiji vya jirani kukutana na
Chukua Hatua. Ni rafiki waliyekutana naye mwaka 2011 katika mazungumzo maalumu
ambayo walitakiwa kuyafikisha kwa wananchi wenzao wa vijiji vya Shenda, Iponya,
Nyakasumula na Bukandwe katika wilaya ya Mbogwe mkoani Geita. Ni katika mazungumzo hayo ya siku tatu,
ambayo Fedson toka kijiji cha Shenda alibadilishwa na kuwa mraghbishi wa
aling’amua uwezo alio nao katika kusimamia rasilimali za kijiji chao, suala ni angezisimamiaje
wakati yeye si kiongozi na ni jukumu la wanakijiji
wote. Katika mazungumzo hayo rafiki yao, Chukua Hatua aliwaambia, “Ni jukumu lako
Fedson na waraghbishi wengine mliopo hapa, ni jukumu lenu la msingi kuj i t aj
i r i sha kwa taarifa na maarifa. Kwa kufanya hivyo mtakuwa na uwezo wa kujenga
hoja mkizithibithisha na vielelezo. Hivyo ni jukumu lenu kujua ni wapi na toka
kwa nani mtapata taarifa na vielelezo vya hoja yenu. Uzito wa hoja na maelezo
kwa uthibitisho ni silaha muhimu kama mnataka kushawishi wenz e n u k u c h u k u a hatua.” Baada ya maelezo hayo walitakiwa kwenda
kutembelea halmashauri ya wilaya yao, wakati huo ikiitwa Bukombe. Na baadhi ya maeneo
hayo ni ofisi za Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri. Maelezo haya yalilenga
katika haki ya kupata taarifa, kwa mujibu wa ibara ya 18 ya Katiba.
“Kweli mazungumzo hayo
yalinijengea uwezo mkubwa sana, Chukua Hatua alinipatia muongozo na akanipangia
kwenda kwa mkuu wa wilaya. Moja kwa moja nikaonana na DC nikaanza kumuhoji
mambo mbalimbali kuhusu pembejeo. Ingawa majibu aliyonipa sikuridhika nayo, lakini
nilishukuru kupata nafasi ya kuongea naye. Na kwa kweli tokea siku hiyo nikawa
na ujasiri mkubwa sana,” Fedson Yaida akitoa ushuhuda wa siku ambayo uoga ulimtoka.
yalinijengea uwezo mkubwa sana, Chukua Hatua alinipatia muongozo na akanipangia
kwenda kwa mkuu wa wilaya. Moja kwa moja nikaonana na DC nikaanza kumuhoji
mambo mbalimbali kuhusu pembejeo. Ingawa majibu aliyonipa sikuridhika nayo, lakini
nilishukuru kupata nafasi ya kuongea naye. Na kwa kweli tokea siku hiyo nikawa
na ujasiri mkubwa sana,” Fedson Yaida akitoa ushuhuda wa siku ambayo uoga ulimtoka.
Ujasiri huo wenye msukumo wa ndani
toka kwa mraghbishi mmoja kwenda kwa wenzake kwa njia ya kuwashirikisha aliyopatiwa
na Chukua Hatua, ndio umekuwa chanzo kikubwa cha mafanikio ya pamoja ya wana
Shenda katika kusimamia rasilimali zao. Safari ya mwandishi katika kijiji cha Shenda
ilimtia moyo sana. Alikutana na waraghbishi toka vijiji vya Shenda, Ipoja, na Buluhe.
Mkusanyiko huu ulikuwa na watu wa kada mbalimbali; walimu, wajumbe wa serikali ya
kijiji, wazee, na wakulima. Aliwakuta wakiwa pamoja na Mwenyekiti na Mtendaji
wa kijiji chao. Na wote kwa pamoja walikuwa wanazungumzia mustakabali wa
maendeleo ya kijiji chao. Na kwa haraka aligundua wote wamekuwa waraghabishi,
akajiuliza aliyekutana na Chukua Hatua alikuwa mmoja, lakini sasa wapo kwa
makundi na wote wanajitambulisha kama waraghbishi. Hamu na shauku yao ya kutaka kusimamia rasilimali
zao ndio imekuwa nguzo kubwa ya wao kuweza kufuatilia matumizi ya vyanzo vya
mapato ya kijiji chao. Ni miaka miwili imepita toka wananchi hao wautoe uongozi
wa kijiji madarakani kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha. Kwa pamoja waliongozana
na mwenyekiti wao pamoja na mtendaji wa kijiji na mpaka ofisi ya kata na
kuwakabidhi kwa polisi. Ubadhirifu huo ulithibitishwa na taarifa ya ukaguzi,
iliyoonyesha upotevu wa kiasi cha shilingi milioni mbili laki tisa na elfu hamsini
(2,950,000/-). Taarifa hiyo ilisomwa katika mkutano wa hadhara na viongozi
kutakiwa kulipa pesa hizo ambazo walizirudisha.
toka kwa mraghbishi mmoja kwenda kwa wenzake kwa njia ya kuwashirikisha aliyopatiwa
na Chukua Hatua, ndio umekuwa chanzo kikubwa cha mafanikio ya pamoja ya wana
Shenda katika kusimamia rasilimali zao. Safari ya mwandishi katika kijiji cha Shenda
ilimtia moyo sana. Alikutana na waraghbishi toka vijiji vya Shenda, Ipoja, na Buluhe.
Mkusanyiko huu ulikuwa na watu wa kada mbalimbali; walimu, wajumbe wa serikali ya
kijiji, wazee, na wakulima. Aliwakuta wakiwa pamoja na Mwenyekiti na Mtendaji
wa kijiji chao. Na wote kwa pamoja walikuwa wanazungumzia mustakabali wa
maendeleo ya kijiji chao. Na kwa haraka aligundua wote wamekuwa waraghabishi,
akajiuliza aliyekutana na Chukua Hatua alikuwa mmoja, lakini sasa wapo kwa
makundi na wote wanajitambulisha kama waraghbishi. Hamu na shauku yao ya kutaka kusimamia rasilimali
zao ndio imekuwa nguzo kubwa ya wao kuweza kufuatilia matumizi ya vyanzo vya
mapato ya kijiji chao. Ni miaka miwili imepita toka wananchi hao wautoe uongozi
wa kijiji madarakani kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha. Kwa pamoja waliongozana
na mwenyekiti wao pamoja na mtendaji wa kijiji na mpaka ofisi ya kata na
kuwakabidhi kwa polisi. Ubadhirifu huo ulithibitishwa na taarifa ya ukaguzi,
iliyoonyesha upotevu wa kiasi cha shilingi milioni mbili laki tisa na elfu hamsini
(2,950,000/-). Taarifa hiyo ilisomwa katika mkutano wa hadhara na viongozi
kutakiwa kulipa pesa hizo ambazo walizirudisha.
0 comments: