Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(SUMATRA),Gilliard Ngewe akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ushushwaji wa nauli za mabasi ya masafa marefu ofisini kwake jijini Dar es salaam leo.
kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Udhibiti usafiri wa barabara,Geffrey Silinda akifafanua jambo kwa waandishi wa habari katika ofisi za Mamlaka ya Uthibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) leo jijini Dar es Salaam,kulia ni Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(SUMATRA),Gilliard Ngewe.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(SUMATRA) leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii)
Na Bakari Issa,Globu ya jamii.
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini(SUMATRA) imeshusha nauli za mabasi ya masafa marefu huku nauli za daladala viwango vyake vikibaki kama kawaida.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA),Gilliard Ngewe wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es salaam leo.
Ngewe amesema uamuzi huo umekuja baada ya mamlaka hiyo kufanya utaratibu wa kupitia kanuni kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo watoa huduma ili kutoa maoni yao,kutokana na ongezeko la msongamano wa magari mijini.
0 comments: