Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran amesema kuwa kitendo cha kinyama cha magaidi cha kuwaua shahidi
Waislamu katika mji wa Hilla ambao walikwenda nchini Iraq kuzuru Haram
ya mjukuu wa Mtume Muhammad (saw), Imam Hussein (as) kinaonesha upeo wa
juu wa kubakia nyuma kwa wahalifu hao wenye nyoyo zilizopofuka.
Taarifa iliyotolewa na Rais Rouhani kuhusu uhalifu huo imelaani
shambulizi la kigaidi lililotokea jana katika mji wa Hilla kwenye mkoa
wa Babel nchini Iraq na kusema kuwa: Kufanyika kwa mafanikio hamasa ya
Arubaini ya Imam Hussein bin Ali (as) ni sehemu ya adhama ya mapenzi ya
mataifa ya Waislamu kwa kizazi cha Mtume Muhammad (saw), suala ambalo
haliwezi kuvumiliwa na makatili wenye nyoyo zilizopofuka.
Taarifa ya Rais Rouhani imesema kuwa, shambulizi la kigaidi
lililofanyika katika mji wa Hilla na kuua shahidi makumi ya Waislamu
waliokwenda kuzuru kaburi la Imam Hussein (as) wakiwemo raia wa Iran,
linawaumiza Waislamu wote hususan wafuasi na wapenzi wa Watu wa Nyumba
ya Mtume Muhammad (saw).
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ameitaka serikali ya Iraq kuwashughulikia
ipasavyo watu waliotenda jinai hiyo na kutangaza kuwa Iran iko tayari
kikamilifu kutoa ushirikiano na kuwasaidia watu waliopatwa na maafa
katika tukio hilo. Amesema kuwa serikali ya Iran imeazimia vilivyo
kufanya mapambano ya pande zote dhidi ya magaidi na makundi yenye
misimamo ya kufurutu mipaka na kuongeza kuwa, hivi karibuni dunia
itashuhudia ushindi wa mwisho wa taifa la Iraq katika mapambano yake na
makundi ya kigaidi na waungaji mkono wao.
Mlipuko wa gari lililokuwa limetegwa mabomu katika kituo cha mafuta
ya petroli katika eneo la al Shomali huko Hilla nchini Iraq umeua
shahidi karibu Waislamu 100 waliokwenda kufanya ziara ya Imam Hussein na
kujeruhi wengine zaidi ya 20. Makumi ya mashahidi waliouawa katika
shambulizi hulo la kigaidi ni raia wa Iran.
No comments:
Post a Comment