Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole (kwa niaba ya Watanzania) kufuatia taarifa ya kifo cha Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis kilichotokea jumatatu ya pasaka tarehe 21, April 2025.
Latest Articles
TANZIA: MHE.RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA POLE KIFO CHA PAPA FRANCIS
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:58 AMRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole (kwa niaba ya Watanzania) kufuatia taarifa ya kifo cha Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis kilichotokea jumatatu ya pasaka tarehe 21, April 2025.
Rais Samia ameandika "Nimesikitishwa na taarifa ya kifo cha Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francisko. Katika kipindi chote cha miaka 12 akiwa Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francisko ameishi maisha yake kama mwalimu na kiongozi aliyefundisha na kuhimiza ustawi na maendeleo ya watu pamoja na kudumisha amani"
Dkt Samia ameongeza
"Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninatuma salamu za pole kwa waumini wote wa Kanisa Katoliki hapa nchini na duniani kote."
Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema Peponi.
Amiina
read more
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe.Japhet Hasunga akizungumza wakati wa kikao mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa mabweni ya wanafunzi ( Hosteli) unaotekelezwa na Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Machi 25,2025 Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.
...........
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imeipongeza Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) kwa matumizi sahihi ya FORCE akaunti yenye kuleta tija kwenye miradi mbalimbali nchini.
Pongezi hizo zilitolewa Machi 24, 2025 Jijini Arusha, na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Japhet Hasunga mara baada ya kamati kukagua ujenzi wa mradi wa mabweni ya wanafunzi.
Aidha Kamati hiyo pia imepongeza NM-AIST kwa kuzalisha bunifu110 huku bunifu 22 zikipata hati miliki na kusisitiza bunifu hizo kubishwarishwa ili kuleta tija zaidi katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) pamoja na nchi nyingine zinazofika kujifunza kuhusu masuala ya bunifu.
Vilevile, kamati hiyo imeiagiza NM-AIST kuhakikisha inaendelea kufanya bunifu ikiwemo kuzisajili kwa kupata hati miliki ili kuepuka Teknolojia hizo kuibiwa zinazogunduliwa na wabunifu.
Mhe. Hasunga alisema, endapo bunifu hizo zikitoa matokeo ya bunifu upatikanaji wa hati miliki utasaidia wabunifu kutoibiwa mawazo yao sanjari na kuziuza ili wahusika waweze kupata kipato na kujikwamua kiuchumi.
"Bunifu zenu hakikisheni zinaingia sokoni lakini pia tunawapongeza kwa muonekano wa thamani halisi ya fedha za mradi huu ikiwemo matumizi ya force akaunti" Mhe.Hasunga
Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Profesa Maulilio Kipanyula ambaye ni Makamu Mkuu wa Taasisi hiyo, alisema jengo hilo la mabweni pacha matatu lina thamani ya sh bilioni 6.109 likiwa na vyumba 184 ambapo vyumba 160 ni vya kujitosheleza na vyumba 20 ni vya mfano wa apatimenti kwa ajili ya kinamama wenye watoto pamoja na vyumba vinne kwa ajili ya matumizi mtambuka.
Prof Kipanyula alisema mradi huo wa mabweni pacha matatu umefikia asilimia 74 na unatarajia kukamilika Juni 30, 2025 ambapo lengo kuu la taasisi hiyo, ni kutoa mafunzo ikiwemo utafiti ambapo hadi sasa kuna wanafunzi kutoka nchi 16 tofauti za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Kusini mwa j Nangwa la Sahara wanasoma katika taasisi hiyo.
Kuhusu ufafanuzi wa bunifu ya inzi lishe , Naibu Makamu Mkuu ,Taaluma,Utafiti na Ubunifu Profesa Anthony Mshandete alisema inzi chuma huyo ni nzi asiyeambukiza na hutaga mayai zaidi ya 500 ambayo huzilisha funza lishe kwa ajili ya kutengeneze chakula cha mifugo na mbolea.
Alisema uzalishaji wake unajali mazingira ikiwemo uchafu unaozalishwa na zao la mkonge kubuniwa na hatimaye kupata chakula hicho cha mifugo na mbolea rafiki kwa wakulima.
Awali wabunge wa kamati hiyo akiwemo, Mhe. Isack Kamwelwe mbunge wa Katavi na Mhe. Condester Sichalwe kutoka Momba walipongeza taasisi hiyo, kwa kufanya bunifu mbalimbali na ufanisi wa mradi wa bweni hilo ikiwemo mandhari nzuri ya taasisi hiyo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe.Japhet Hasunga akizungumza wakati wa kikao mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa mabweni ya wanafunzi ( Hosteli) unaotekelezwa na Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Machi 25,2025 Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo akiongea jambo wakati wa kikao na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali ( PAC) iliyofanya ziara ya kutembelea na kukagua Mradi wa Ujenzi wa Bweni la Wanafunzi katika Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Machi 25,2025 Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Balozi Maimuna Tarish akizungumza wakati wa kikao na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) waliofanya ziara ya kukagua na kutembelea mradi wa ujenzi wa Bweni la Wanafunzi wa Taasisi hiyo, Machi 25,2025 Kampasi ya Tengeru jijini Arusha. 

Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi wa mabweni ya wanafunzi kwa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) , Machi 25,2025 kampasi ya Tengeru Jijini Arusha.





Wajumbe wa Menejimenti ya Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) wakiwa katika cha kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) mara baada ya ziara ya kukagua Mradi wa Ujenzi wa Bweni la Wanafunzi Machi 25,2025 Kampasi ya Tengeru jijini Arusha.
read more
WAZIRI MKUU AAGIZA KITUO CHA AFYA MAMA NGOMA KUPANDISHWA HADHI.
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:45 AMWAZIRI MHAGAMA AWASILISHA UJUMBE MAALUM WA RAIS SAMIA KWA RAIS CHAKWERA WA MALAWI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:35 AMWaziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama leo Machi 26, 2025 amewasilisha ujumbe maalum wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Rais wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Lazarus Chakwera katika Ikulu ya Rais iliyopo Jijini Lilongwe, Malawi.
Rais Chakwera amemshukuru Rais Samia kwa ujumbe huo maalum na kubainisha ya kuwa Malawi na Tanzania zitaendeleza ushirikiano wa kihistoria uliopo baina ya mataifa hayo mawili.
Waziri Mhagama akiwa ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Malawi Mhe.Agnes Kayola pamoja na ujumbe wake amemshukuru Rais Chakwera kwa mapokezi mazuri na kusema kuwa Rais Samia anashukuru na kutambua umuhimu wa kuendeleza mahusiano mazuri ya kidiplomasia kati ya Tanzania Malawi ambayo yanawanufaisha raia wa nchi zote.
MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO MGENI RASMI UZINDUZI WA MWENGE
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:26 AM
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi na Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete (MB) pichani leo alipotembelea Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha Mkoani Pwani na kuridhishwa na maandalizi yaliyofikia kwa asilimia 95
Na Khadija Kalili Michuzi TV
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Philip Isidory Mpango atazindua mbio za Mwenge wa Uhuru tarehe 2 Aprili 2025.
Akizungumza leo tarehe 26 Machi 2025 kwenye mkutano na Waandishi wa Habari Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Vijana , Ajira na Wenye Ulemavu Mhe.Ridhiwani Kikwetete (MB) alipozungumza kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Pwani.
"Awali ya yoye napenda kutumia fursa hii kumshkuru Mungu kwa kurukutanisha siku ya leo tunapoelekea katika tukio la uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025" amesema Kikwete.
"Napenda kutoa taarifa kwa umma kuwa uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru utakuwa katika Uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha, Mkoani Pwani" amesema Kikwete.
Waziri Kikwete ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mkoani Pwani amesema kuwa baada ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025 kuzinduliwa Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango atawakabidhi vijana sita waliochaguliwa kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, watakaokuwa na jukumu la kukimbiza Mwenge wa Uhuru katika Mikoa 31 yenye jumla ya Halmashauri 195 za Jamhuri ya Muungano wa Tanza kwa siku 195 na katika kipindi hicho chote,Mwenge wa Uhuru utafanya kazi ya kuhamasisha amani, umoja upendo na mshikamano wa Kitaifa .Vilevile Mwenge wa Uhuru utawahimiza wananchi kushiriki.shughuli za maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika maeneo yao ya Halmashauri.
Kauli mbiu mwaka huu umebeba kaulimbniu isemayo 'Jitokeze kushiriki uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu 'ujumbe wa Mwenge wa mwaka huu unalenga kuwaelimisha na kuwaunganishs wananchi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushiriki kikamilifu katika uchaguzi Mkuu kwa amani utakaofanyika mwaka huu.
Aidha Mwenge wa Uhuru utatumika kuelimisha wananchi katika maeneo yote nchini juu ya masuala ya kisekta na katika muktadha wa Kitaifa na Kimataifa ikiwa ni pamoja na maradhi yanayotishia ustawi wa watu kama vile UKIMWI, Malaria na kupambana na matumizi ya Dawa za Kulevya na Vitendo vya rushwa .Vilevile katika Halmashauri zote utakapokuwa Mwenge wa Uhuru utaendelea kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa Lishe Bora kwa afya imara.
Mwaka 1961 Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliuwasha Mwenge wa Uhuru na kumkabidhi Mwenge wa Uhuru na Bendera ya Taifa Luteni Alexander Ngweba Nyirenda na kikosi cha vijana wenzake wakaupandisha Mwenge wa Uhuru na Bendera ya Taifa la Tanganyika juu ya Mlima Kilimanjaro. Mwalimu Nyerere wakati akitoa hotuba ya siku ya Uhuru aliwatangazia Watanganyika , Afrika na Dunia kwa ujumla kwa kutamka maneno haya"Sisi tumekwisha uwasha Mwenge wa Uhuru na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, umulike ndani na nje ya mipaka yetu,ulete matumaini pale ambapo hakuna matumaini,ulete upendo mahali penye chuki na heshima mahali penye dharau" amesema Mhe.Kikwete.
"Watanzania wenzangu tunatambua kuwa falsafa hii ya Mwenge wa Uhuru, ndiyo chimbuko la Mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya Mwaka 1964,Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wa mwaka 1964 na Azimio la Arusha la mwaka 1967.Niwasisitize watanza tuendeleze Mwenge wa Uhu kama ulivyo asisiwa na Hayati Mwalimu Julius Kambarage mwaka 1961 wakati Taifa letu lilipopata Uhuru" amesema.
"Napenda kutoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Pwani,Mikoa ya jirani na watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi"amesema Mhe.Kikwete.
read more
KITUO KIPYA CHA AFYA CHA CURE SPECIALIZED POLYCLINIC CHAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM.
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:17 PMBaadhi ya Waalikwa wakiwa kwenye uzinduzi wa Kituo hicho.
Dk. Hamisa Iddy Khamis akitoa utangulizi na utambulisho wakati wa uzinduzi wa kituo hicho.
Mkurugenzi wa Tiba na mtaalam wa utoaji huduma za Lishe Dr. Rehema Mzimbiri akizungumza na baadhi ya Waalikwa waliofika katika uzinduzi wa Kituo hicho.
Mkurugenzi wa Tiba na mtaalam wa utoaji huduma za Lishe Dr. Rehema Mzimbiri akikata Utepe kwa ishara ya Uzinduzi wa The Cure Specialized Polyclinic, eneo la Upanga Jijini Dar es Salaam, leo Jumamosi, Januari 4, 2025. Kulia ni madaktari wa kituo hicho.
Akizungumza mwishoni mwa hafla hiyo, Dr. Mbobezi wa Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu wa The Cure Specialized Polyclinic Dk. Juma Magogo Mzimbiri, alisema kituo hicho kina uwezo wa kupokea wagonjwa hadi 50 kwa siku.
Baadhi ya Madaktari wakiwa katuika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi
read more
Akizungumza mwishoni mwa hafla hiyo, Dr. Mbobezi wa Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu wa The Cure Specialized Polyclinic Dk. Juma Magogo Mzimbiri, alisema kituo hicho kina uwezo wa kupokea wagonjwa hadi 50 kwa siku.
Baadhi ya Madaktari wakiwa katuika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi
WAZIRI WA HABARI. UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO, MHE. PROF. PALAMAGAMBA KABUDI LEO AJITAMBULISHA KWA WADAU WA SEKTA YA HABARI NA UTANGAZAJI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:46 PM
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi .akizungumza wakati alipokuwa akijitambulisha kwa Wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji leo Desemba 18, 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA) wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (pichani hayupo) wakati alipokuwa akijitambulisha kwao leo Desemba 18, 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (pichani hayupo) wakati alipokuwa akijitambulisha kwao leo Desemba 18, 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akizungumza na wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji (pichani hawapo) leo Desemba 18, 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi leo 18, Desemba 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi leo 18, Desemba 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
read more
wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji wakimsikiliza Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (pichani hayupo) wakati alipokuwa akijitambulisha kwao leo Desemba 18, 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akizungumza na wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji (pichani hawapo) leo Desemba 18, 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi leo 18, Desemba 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi leo 18, Desemba 2024 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
read more
Subscribe to:
Posts (Atom)