Latest Articles

DCI MSTAAFU BALOZI ADADI RAJAB OCTOBA 29 TUJITOKEZENI KWA WINGI KUPIGA KURA

 -Awataka watanzania kutoka kwa wingi kupiga kura kumchagua Dkt Samia Suluhu,Wabunge na Madiwani wanaotokana na CCM.


Na Oscar Assenga,MUHEZA.

MKURUGENZI Mstaafu wa Makosa ya Jinai nchini (DCI) Balozi Adadi Rajabu amesema kwamba suala la amani na utulivu ni muhimu Octoba 29 mwaka huu kupiga kura huku akiwataka watanzania kujitokeza kwa wingi na kwamba siku hiyo hakutakuwa na maandamano yoyote kutokana na uimara wa vyombo vya ulinzi hapa nchini.
 

Balozi Adadi aliyasema hayo wakati wa mkutano wa kampeni wa kumnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Hamisi Mwinjuma alimaarufu Mwana FA katika halfa ambayo mgeni rasmi alikuwa ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajabu Abdurhamani ambapo alisema suala la amani ni muhimu sana

Alisema kwamba anasema hayo kutokana na kwamba yeye amekulia kwenye vyombo na anajua vyombo hivyo vinafanya nini vipo kwenye mazoezi kuangalia wale ambao wataleta chokochoko Octoba 29 washughulike nao.
“La mwisho suala la amani na utulivu Octoba 29 ni muhumu kuna watu wametokea wanaleta chochoko kwenye mitandano kwamba kuchafua na maandamano nawahakikishia hakutakuwa na maandamabo vyombo vipo imara”Alisema

“Niwaambie kwamba mimi nimekulia kwenye vyombo na najua vyombo vinafanya nini vipo kwenye mazoezi kuangalia wale ambao wataleta chokochoko Octoba 29 nawaomba mtokea kwa amani ikiwemo misusuru ya kwenda kwenye vituo vya kupigia kura mimi nitapiga kura Kerenge”Alisema

Aidha alisema kwamba baada ya kupiga kura ataangalia hali ya usalama inaende vipi hivyo kuwataka watoke wasiwe na hofu yoyote kwamba kutakuwa na watu gani ambao watawashauri waangamane wewe umeshaona watu wa aina hiyo.
“Vitu vya namna hii havijawahi kutokea sijaona mimi kulikuwa na ndugu zangu Waislamu miaka nipo kazini kulitokea maandamano mengi kule Magomeni kwa hiyo wachache wakafungwa ,wachache wakaenda jela”Alisema

Alisema kwamba lakini wale walivyotoka jela wakasema yale yalikuwa ni mambo ya kipumbavu wenzao waliwauza kuna wenzao waliwauza wao hawakutokea walikaa nyuma nyuma wao walikuwa mbele wakadakwa wakafungwa na kueleza hawarudiii tena hilo ni somo hivyo wapige kura kwa amani na utulivu bila matatizo yotote .

Balozi Adadi aliwambia wana Muheza katika mkutano huo kwamba wana kila sababu ya kumchagua Dkt Samia Suluhu kwa sababu ya mambo ambayo ameyafanya katika kipindi cha miaka minne kipovu haambiwa tazama ukiangalia malengo kila upande samia amegusa na uchumi umeongezekana na upo juu ukiangalia sekta ya miundombu barabara za lami nchi nzima.
Alisema pia ukiangalia ndege ambazo zimekuja zipo zaidi ya 15 pamoja na treli ya SGR watu siku hizi wanalala Dodoma wanakwenda kufanya kazi Dar huku wanalala Morogoro wanakwenda kufanya kazi Dar yote ni uchumi kuongezeka kwa kasi,.

Akizungumzia watalii alisema kwamba yeye alikuwa Balozi nchini Zimbabwe kivutio cha utalii ni kimoja tu Victoria Falls wale walikuwa wanaingiza watalii 2,500 na Samia Suluhu alivyoingia madarakani hapa nchini kuna vivutio vingi sana pamoja na vyote hivyo lakini watalii ambao walikuwa wanaingia walikuwa hawafiki Milioni 1 sasa hivi baada ya Royal Tour na sio raisi kufanya hivyo.

Alisema lakini Dkt Samia Suluhu alivunja rekodi aliingia na kufanya filamu ya hiyo na sasa wanaingiza watalii Milioni 5 na nusu lakini pia amefanya mambo mengi sana na uchumi umepanda kwa kiasi kikubwa sana na hata mfumuko wa bei upo katikati ni kitu cha kujivunia.

Hata hivyo aliwaomba wananchi wa Jimbo la Muheza kumchagua Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo (CCM) Hamisi Mwijuma alimaarufu Mwana FA kwa sababu ni Mbunge k mwenye uwezo wa kila kitu na hatuwezi kuwa na mbunge anakuwa njaa badala ya yeye kuombwa yeye anaomba.

“Jamani Muheza tunahitaji Mbunge kama huyo ?hatuwezi kuwa na mbunge ambaye anaambiwa zahanati haijapauliwa anagonjea fedha ya Serikali sasa si kichekesho hicho,”Alisema

Balozi Adadi alisema kwamba anamuona mwana FA ndio mbunge ambaye anaweza kuongoza wilaya ya Muheza kutokana na uwezo wake akiingia bungeni sio bubu wala kukaa mjengoni kwani kuna wabunge wana lala miaka 5 hawajafungua mdomo.

“Mimi sikugombea safari hii na sidhani kama nitagombea tena lakini nilimuita mwana FA tukaongea yeye ndio anastahili kushika Jimbo la Muheza yeye ndio mwenye uwezo yeye akiingia bungeni sio bubu wala kukaa mjengoni kuna wabunge wengine wana lala miaka 5 hajafungua mdomo kuzungumza”Alisema

Aliwataka wana Muheza wamuombee ili aweze kuingia tena mjengoni aweze kuchaguliwa kuwa Waziri hiyo ni sifa ya Muheza unapokuwa waziri unakuwa na Faida na una uwezo wa kuongea na Mawaziri wenzake ,makatabu wakuu wowote ili Muheza iweze kupata msaada.

Hata hivyo alisema kwamba hata mbunge anatakiwa awe na nguvu ya kugonga kokote na hawahitaji wabunge waoga waoga hivyo lakini pia chagueni na madiwani ambao ni mahiri ambao wanaendea kutuletea maendeleo.
read more

WAKILI MAHAKAMA KUU YA TANZANIA KUFUNGUA KESI KWA NIABA YA WANANCHI KUHUSU TOZO DARAJA LA KIGAMBONI

    Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mohamed Majaliwa

WAKILI wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mohamed Majaliwa amesema kwa niaba ya wananchi wa Kigamboni anakwenda kufungua kesi ya Kikatiba kuomba Mahakama itoe tamko kwamba kulipa tozo la Daraja la Kigamboni ni kinyume cha Katiba.


Wakili Majaliwa amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusiana na mchakato wa kufungua shauri la Kikatiba Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam.


Amesema wamefikia hatua hiyo, baada ya kutumia mbinu mbalimbali ya kumaliza tatizo hilo lakini imeshindikana, wameamua kwenda kisheria zaidi ili kuondoa changamoto hiyo.


"Tunakwenda kufungua kesi kwa kuomba Mahakama itoe tamko tu kwamba kitendo cha wananchi wa Kigamboni au mwananchi yeyote kutoka nje ya Kigamboni kutaka kuvuka kuingia kulazimika kulipa tozo ya daraja ni kinyume na Katiba,"


"Na hasa kuzingatia juzi wastani wa mwezi mmoja umepita nilikuwa nimefuatilia uzinduzi wa Dira ya Maendeleo ya miaka 25 mbele sijaona nafuu kwa watu wa Kigamboni kuondosha tozo zile, "Amesema Wakili Majaliwa.


Amesema utaratibu unaoendelea wa tozo hizo, unakizana na sheria zenyewe, sheria ambazo zinatumika kutoza tozo zipo za aina mbili, The Road Tolls (Fees) Regulations, 1985 (Kanuni ya tozo za barabara) na The Road and Fuel Tolls Act (Sheria ya tozo za barabara na mafuta). 


"Ukizisoma sheria hizi mbili kwa pamoja kwa ujumla wake, mimi mwananchi wa Kigamboni nikitumia daraja kwa kuvuka kwa daladala au gari yangu binafsi naangukia katika kulipa kodi mara mbili,"amesema

read more

DK. SAMIA AWATAKA VIJANA KUIPENDA NCHI YAO

 MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ametoa rai kwa vijana nchini wasikubali kudanganyika ili kuchafua amani ya nchi.

Akizungumza leo katika viwanja vya TANESCO -Buza villivyopo Wilaya ya Temeke mkoani Dar es Salaam akihitimisha mikutano yake ya kampeni za uchaguzi mkuu, Dk. Samia ametumia nafasi kuwaeleza vijana umuhimu wa kutunza amani iliyopo nchini.

Amesisitiza kwamba Tanzania ni eneo sahihi kwa vijana kuishi tofauti na maeneo mengine Afrika, hivyo amewataka wasikubali kufanganywa kwa namna yeyote ili kuvuruga amani ya nchi yao.

"Hapa mpo kwenye nchi yenye jina, yenye sifa zake, yenye kuendeleza watu wake. Msidanganywe wale ambao wapo nje wasiwadanganye. 

“Hapa mpo pazuri kweli kweli.Niwahakikishie vijana wa Tanzania, hawa wazee wenzangu wanaelewa. Vijana wa Kitanzania msidanganywe, ukichukua Afrika Mashariki, Kusini na Kati, Tanzania ni pepo.Nchi yetu iko salama”

Akisisitiza zaidi Mgombea Urais Dk.Samia amesema "Mkipata fursa kuingia kwa majirani zetu, mtaona vijana wenzenu wanavyokula ngumu. Mtasema mnataka kurudi kwenu."

Amewakumbusha kuwa vijana ndio wanategemewa kukabidhiwa nchi kuiendesha kama inavyoendeshwa bila kudanganywa.”Katika kuongoza nchi, taifa limeweka mifumo mizuri ya kidemokrasia kwa kuchaguana kila baada ya miaka mitano.”

"Tulizeni munkali, nchi hii ni mali yenu, hakuna mwenye cheti anayesema nchii hii ni mali yangu. Sisi tunawakilisha wananchi, wananchi ndiyo nyinyi.Hakuna mwenye miliki ya wananchi, wananchi ndiyo nyinyi. 

“Tumepeana tu majukumu, niwaombe sana vijana msiharibu nchi yenu. Fuateni serikali yenu inavyowaambia, fuateni katiba yenu inavyowaelekeza," amesema Dk.Samia.

Pamoja na hayo ametoa mwito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kupigakura kwani ndiyo haki ya msingi kidemokrasi.

“Hakuna mfumo uliowekwa kuhusu siasa safi kwani siasa safi ni kuhakikisha nchi na wananchi wapo salama ikiwemo kujumuishwa katika maamuzi.

“Serikali imekuwa ikiunda kamati kukusanya maoni kuhusu masuala mbalimbali yenye kuhusu maendeleo ya nchi.Hata panapotokea mazonge kwenye nchi tunaunda tume kuja kuwauliza, mnatoa maoni yenu. Hiyo ndiyo siasa safi.”

Ameongeza kuwa “Mnapokerana mnaitana kuzungumza, tuyazungumze, tuelewane, twende pamoja hiyo ndiyo siasa safi.”Amesema Dk.Samia na kuongeza  hayo ndiyo mambo Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere aliyokuwa akiyasimamia ambapo serikali zote za CCM zimekuwa zikitekeleza.












read more

MOHAMED ABDALLAH: MTAMBILE YAJAA FURAHA NA IMANI KWA CCM

 

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Mtambile, Mkoa wa Kusini Pemba, Mheshimiwa Mohamed Abdallah Kassim, kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema kuwa hali ya kisiasa katika jimbo hilo ni ya amani na furaha, kwani ni sherehe za ushindi ndizo zinaendelea, siyo maandamano.

Akizungumza katika mwendelezo wa kampeni za CCM zinazoendelea jimboni humo, Mheshimiwa Mohamed alisema wananchi wa Mtambile wameonyesha imani kubwa kwa chama hicho na wako tayari kuipa ushindi mkubwa katika uchaguzi ujao.

“Wananchi wa Mtambile wanajua mazuri yaliyofanywa na serikali ya CCM chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Hivyo, ni furaha na shangwe za ushindi zinazotawala, hakuna dalili yoyote ya maandamano,” alisema.

Aidha, aliwataka wananchi waendelee kuiamini CCM kwa kuwa ni chama pekee kilichoonyesha uthabiti katika kuwaletea maendeleo Watanzania wote bila ubaguzi.

“Naomba tuendelee kushikamana, tuiunge mkono CCM kupitia kura zetu, kwani kwa pamoja tutaendelea kusonga mbele katika maendeleo,” alisisitiza.

Mheshimiwa Mohamed aliongeza kuwa wananchi wa Mtambile wako tayari kumpa kura Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Rais wa Zanzibar na Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ili waendelee kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

read more

WATENDAJI WA UCHAGUZI WAKUMBUSHWA KUSHIRIKIANA NA WANAHABARI

  Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira amewakumbusha watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Mkoa na Jimbo kushirikiana na Wanahabari ili wananchi waweze kufahamu mambo mbalimbali yahusuyo Uchaguzi.


Wito huo ameutoa leo alipokuwa akifunga mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Mkoa na Jimbo yaliyofanyika kwa siku tatu katika Kituo cha Tabora yaliyojumuisha watendaji kutoa Mikoa wa Tabora na Kigoma.

"Katika utekelezaji wa majukumu yenu, mtapaswa kutoa taarifa mbalimbali kwenye vyombo vya habari ili kuwajulisha wananchi na wadau wa Uchaguzi mambo mbalimbali yanayohusu Uchaguzi" alisema Mhe.Rwebangira.

Aidha Mhe.Rwebangira amewasisitiza watendaji hao kuhakikisha wanatunza rasilimali vifaa vya Uchaguzi watavyovipokea kwaajili ya Uchaguzi sambamba na kuhakikisha wanafuata Sheria, kanuni na miongozo kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili wakatimizie jukumu la usimamizi wa Uchaguzi kwa weledi.

Mafunzo haya ya siku tatu yenye lengo la kuwajengea uwezo watendaji wa Uchaguzi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 yamekamilika leo tarehe 17 Julai, 2025.
read more

BENK YA NMB NA OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI ZAIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA UTOAJI WA HUDUMA KWA WATEJA

  Ujumbe kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (OAG) ukiongozwa na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Samwel M. Maneno, umetembelea makao makuu ya Benki ya NMB na kufanya kikao na uongozi wa benki hiyo ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu, Bi. Ruth Zaipuna.

Kikao hicho kilichofanyika katika makao makuu ya NMB jijini Dar es Salaam, kikilenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili, hususan katika kubadilishana uzoefu na mbinu bora za utoaji wa huduma kwa wateja.

Ujumbe wa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali uliambatana na viongozi mbalimbali wakiwemo Bw. Ipyana Mlilo – Mkurugenzi Msaidizi Uratibu, Bi. Leila Muhaji – Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Bw. Juma Mziray – Afisa TEHAMA Mwandamizi, na Bw. Nyamhanga Nyamhanga – Wakili wa Serikali.

Kupitia mazungumzo hayo, pande zote mbili zilitambua umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya sekta ya umma na binafsi katika kukuza ufanisi wa utoaji huduma na kuleta maendeleo jumuishi.

Kikao hicho ni sehemu ya juhudi za pamoja za kuimarisha utawala bora na kuhimiza matumizi ya teknolojia katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi. 




read more

MISS WORLD NA MISS AFRICA WATEMBELEA WODI YA NJITI PAMOJA NA DORIS MOLLEL FOUNDATION

 Wameguswa na kazi kubwa inayofanywa kuwahudumia watoto njiti na wamepongeza juhudi zinazofanyika na kuahidi kuchangia vifaa tiba na kusaidia hospitali nyingine zaidi kwenye maeneo yasiyofikiwa.

read more