KUFICHULIWA UUNGAJI MKONO MPYA WA UTAWALA WA KIZAYUNI KWA MAKUNDI YA KIGAIDI NCHINI SYRIA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 8:45 PM
Katika taarifa yake gazeti la utawala haramu
wa Israel la Haaretz limekiri kwamba Tel Aviv inajishughulisha zaidi na
kuwapatia silaha magaidi nchini Syria.
Kabla ya hapo pia Wizara ya Afya
ya utawala huo wa Kizayuni katika taarifa yake ilitangaza kwamba, zaidi
ya magaidi 1400 waliojeruhiwa na jeshi la Syria, wamepatiwa matibabu
katika hospitali tofauti za Israel. Katika uwanja huo Elizabeth Surcouf,
mtaalamu wa masuala ya kisiasa wa nchini Marekani anayejishughulisha na
matukio ya Syria anasema: "Zaidi ya makundi saba ya kigaidi
yanapata misaada ya silaha, zana za kijeshi na fedha kutoka Israel
kupitia eneo la Golan la nchini Syria. Aidha kabla ya hapo gazeti la The
Wall Street Journal liliripoti kwamba Israel inafanya haraka kuwapatia
silaha na kuyaunga mkono makundi ya kigaidi ya Syria. Kwa mujibu wa
gazeti hilo la Marekani, mwaka 2016 Israel ilianzisha kikosi maalumu cha
kuyapatia misaada tofauti makundi ya kigaidi kama vile silaha, zana za
kijeshi na fedha kwa ajili ya kuwalipa mishahara magaidi hao.” Mwisho wa kunukuu."
Ukweli ni kwamba utawala wa Kizayuni
umekuwa ukishirikiana bega kwa bega na makundi ya ukufurishaji nchini
Syria, huku majeruhi wao, wakitibiwa katika hospitali za Israel ndani ya
ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu. Mashambulizi ya mara kwa
mara ya anga na makombora ya utawala haramu wa Kizayuni dhidi ya maeneo
ya serikali ya Syria, mbali na kwamba yanabainisha wazi uchokozi wa
utawala huo katili, yanaweza pia kutafsiriwa kuwa ni msaada wa kwa
magaidi hao wa Kiwahabi. Kwa hakika hivi sasa Syria inakabiliwa na
mgogoro mkubwa wa ndani unaotokana na njama chafu za madola ya Magharibi
na washirika wao katika eneo pamoja na utawala wa Kizayuni.
Kupitia njama hizo, Israel na madola
hayo ya Magharibi yanayompinga Rais Bashar al-Assad, yanatumia vibaya
baadhi ya malalamiko ya Wasyria kuyaunga mkono kilojestiki makundi ya
kigaidi na yanayofanya ghasia, kwa lengo la kuvuruga usalama na amani ya
nchi hiyo ya Kiarabu. Hata hivyo kipigo ambacho magaidi hao wamekipata
kutoka kwa jeshi shupavu la serikali ya Damascus, kimekuwa na taathira
kubwa katika kudhoofisha uungaji mkono huo wa madola ya Magharibi,
baadhi ya tawala za Kiarabu na utawala wa Kizayuni. Katika mazingira
hayo, Israel inakusudia sambamba na kufanya mashambulizi dhidi ya jeshi
la Syria, iimarishe harakati za makundi ya kigaidi hususan katika maeneo
ya kistratijia ndani ya taifa hilo la Kiarabu.
Ni kwa ajili hiyo ndio suala la
kuongezeka mashambulizi ya utawala wa Kizayuni nchini Syria sambamba na
kuongeza kiwango cha misaada ya Marekani na baadhi ya watawala wa
Kiarabu kwa makundi hayo ya kigaidi, kukawa na maana ya kupewa pumzi
bandia na za mwisho vibaraka wao hao wa kigaidi. Matukio ya Syria
yanaonyesha kwamba, nchi hiyo kwa sasa inakabiliwa na harakati chafu na
za shari, yaani utawala haramu wa Kizayuni na makundi ya kigaidi kupitia
uungaji mkono wa madola ya Magharibi. Ni katika hali hiyo, ndipo wakati
sehemu ya ardhi ya Syria yaani eneo la Golan bado liko chini ya
udhibiti wa utawala wa Kizayuni, nchi hiyo ya Kiarabu inaendelea
kulengwa na hujuma pana za makundi ya kigaidi kwa lengo la kuvuruga
usalama na amani ya taifa hilo. Suala hilo linabainisha njama pana
zinazofanywa dhidi ya nchi hiyo ambayo ina nafasi muhimu ya kistratiji
na moja ya mihimili mikuu ya muqawama katika eneo la Mashariki ya Kati.
Katika uwanja huo, madola ya Magharibi
sambamba na kuzishughulisha nchi za eneo na wimbi la ugaidi, yameongeza
pia njama katika eneo hili ili kwa njia hiyo yaweze kutumia misaada yao
kwa Israel, kufikia malengo yao ya kuibua fitina katika eneo hili
muhimu. Ni kwa kuzingatia kuwa njama hizo zimeratibiwa tangu mapema,
ndio maana tukawa tunashuhudia kiwango kikubwa cha ushirikiano wa
makundi ya kigaidi na utawala haramu wa Israel sambamba na kuongezeka
jinai zao nchini Syria.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: