Israel imewafunga jela Waafrika 7 raia wa
Eritrea walioomba hifadhi katika utawala huo baada ya wakimbizi hao
kukataa kupelekwa Rwanda kwa mabavu.
Taasisi
za kutetea haki za binadamu huko Israel zimeripoti kuwa, wakimbizi hao
wa Kiafrika wamefungwa katika gerezani la Israeli kwa muda mrefu
usiojulikana baada ya kukataa kupelekwa Rwanda.
Wakimbizi
hao ni wa kwanza kufungwa jela tangu utawala haramu wa Israel utangaze
kwamba, utawalazimisha maelfu ya wakimbizi wa Kiafrika kuchagua ama
kuhamishiwa katika nchi nyingine au kufungwa jela kwa muda mrefu
usiojulikana.
Taarifa
iliyotolewa na taasisi mbili za kutetea haki za wakimbizi zenye makao
yao mjini Tel Aviv za Hotline for Refugees and Migrants na ASSAF
imesema: "Hii ni hatua ya kwanza ya operesheni ya kuwahamisha
kwa mabavu wakimbizi kimataifa ambayo haina mfano wake, na ni hatua
inayochochewa na ubaguzi na kudharau uhai na utukufu wa watu wanaotafuta
hifadhi."
Taarifa hiyo imeongeza kuwa, wawili kati ya wakimbizi hao saba wa
Kiafrika ambao wamefungwa katika jela ya Saharonim huko Israel ni
manusura wa mateso.
Wakati
huo huo mamia ya wakimbizi wanaotafuta hifadhi huko Israel walianza
mgomo wa kula chakula jana Jumatano katika kituo cha Holot wanakozuiliwa
wakimbizi hao. Wakimbizi hao wanapinga kitendo cha utawala wa Kizayuni
wa Israel cha kuwafunga jela wenzao saba kutoka Eritrea.
Shirika
la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limetangaza kuwa,
wakimbizi 27,000 kutoka Eritrea na wengine 7,700 kutoka Sudan wameomba
hifadhi huko Israel.
Novemba
mwaka jana utawala haramu wa Israel ulitangaza kwamba, utawasafirisha
wakimbizi walioko katika utawala huo kwa mabavu na kuwapeleka nje. Kwa
mujibu wa vyombo vya habari vya Isarel, wakimbizi hao wanapelekwa kwa
mabavu na bila ya hiari yao katika nchi za Rwanda na Uganda ingawa nchi
hizo mbili zimekanusha kuwa zimefikia makubaliano ya aina hiyo na
utawala haramu wa Israel.
Taasisi za kutetea haki za binadamu zinasema: "Ni jambo la
kushangaza kwa nchi za Rwanda na Uganda kushiriki katika mpango kama huo
na kuiruhusu Israel kuamiliana na wakimbizi wa Kiafrika kwa mabafu,
watu ambao baadhi yao wamekimbia mauaji na udikteta."
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: