UMOJA WA MATAIFA: MAUAJI YA KIMBARI YALIENDESHWA DHIDI YA ROHINGYA BURMA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:26 PM
Bangladesh, wakimbizi wa Rohingya wakipewa mablanketi nje ya kambi ya Kutupalong karibu na Cox's Bazar Novemba 24, 2017.
Mauaji ya kimbari yaliendeshwa dhidi ya jamii ya Waislamu wa Rohingya
nchini Burma. Kauli hii imetolewa katika kikao maalum cha Tume ya Umoja
wa Mataifa ya Haki za Binadamu leo Jumanne (Desemba 5) mjini Geneva.
Kamishna Mkuu Zeid Ra'ad Al Hussein amelaani mashambulizi
yaliyopangwa dhidi ya watu kutoka jamii ya Waislamu wa Rohingya.
Takriban watu 626,000 kutoka jamii hiyo tayari wamekimbilia Bangladesh.
Na idadi hii inaendelea kuongezeka.
Umoja wa Mataifa tayari umelaani jaribio la kuangamiza jamii ya watu
wa Rohingya. Kitendo ambacho kinaendeshwa na viongozi wa nchi hiyo.
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu, Zeid Ra'ad Al Hussein, amekumbusha
madhila yaliowakumba Waislamu kutoka jamii hiyo ya watu wachache nchini
humo.
"Ukichukulia mashtaka ya hivi karibuni ya mauaji, nyumba kuchomwa
huku watu kadhaa wakiwa ndani nyumba hizo, watu kulazimishwa kuyatoroka
makazi yao, ukichukulia pia kuwa Rohyingias inatambulika kama jamii au
kabila ya watu wachache, kwani wana utamaduni wao, na lugha yao... Kwa
vielelezo vyote hivyo, je! kuna mtu yeyote anayeweza kukataa kwamba
hatuna hapa mambo yanayoashiria mauaji ya kimbari? Ninaomba Baraza
kuchukua hatua zote zinazohitajika ili kukomesha kuanzia sasa hali hii, "
Zeid Ra'ad Al Hussein amesema.
Zeid Ra'ad Al Hussein ameomba kuanzishwa kwa utaratibu usio na
upendeleo na wa kujitegemea kuchunguza uhalifu uliofanywa nchini Burma.
Kwa njia ya moja ambayo tayari inashuhudiwa nchini Syria. Viongozi wa
Buram hawataki wachunguzi wa kimataifa katika ardhi yao. Kwa kukabiliana
na mashtaka hayo, mwakilishi wa Burma kwenye Tume ya Umoja wa Mataifa
ya Haki za Binadamu alipendelea kukosoa tuhuma hizo na kuzitaja kuwa ni
hukumu iliyotolewa kimakosa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: