NGUVU YA WANANCHI WA YEMEN, MSINGI WA KUKABILIANA NA NGUVU KUTOKA NJE
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:22 PM
Msemaji wa jeshi la Yemen lenye mfungamano na
Harakati ya Ansarullah ametangaza kuwa, maeneo yote ya mji mkuu Sana'a
yanadhibitiwa na jeshi na kwamba, hali ya usalama ni ya amani na utulivu
kabisa.
Fitina au mapinduzi? Hapana shaka
kuwa, haya ni maneno na istilahi kwa ajili ya kutoa wasifu wa kile
ambacho kilifanywa na rais wa zamani wa Yemen Ali Abdallah Swaleh kabla
ya kuuawa siku ya Jumatatu. Kimsingi sio muhimu kwamba, hatua hiyo
inapewa jina gani, bali la muhimu ni kuwa, mzozo na fitina hiyo
ilimalizika kwa muda mfupi au ilipoteza taathira yake.
Ali Abdallah Swaleh ndiye aliyekuwa
mshindwa mkuu wa fitina hiyo iliyokuwa imeanza Jumamosi iliyopita. Licha
ya kuwa kuna sababu nyingi zinazoweza kutajwa za kushindwa fitina ya
Ali Abdallah Swaleh dhidi ya Ansarullah, lakini moja ya sabahu za
kushindwa huko ni hatua ya Ansarullah ya kutegemea nguvu ya wananchi
ambayo ndio msingi na nguzo.
Ali Karimi, mhadhiri wa Chuo Kikuu
anaamini kwamba nguvu ya wananchi ni nguzo katika Mashariki ya Kati
ambayo inatokana na matukio ya ndani na ya nje katika eneo hili ambayo
huupa changamoto utawala ambao misingi yake inategemea nguvu kutoka nje.
Kimsingi nguvu ya wananchi ni msingi ambao unasimama na kuwa imara kwa
kutegemea uungaji mkono wa wananchi.
Saad Zari'i mtaalamu wa masuala ya kisiasa anaamini kwamba: Usalama
wa wananchi sio msingi wa usalama ambao ni kitu cha pembeni ambacho tawi
lake liko katika nchi fulani na mizizi yake katika nchi nyingine, bali
jambo hilo linatoka katika muundo na moyo wa nchi husika na kwa kuwa
hali iko namna hiyo, basi inawezekana kusimama na kukabiliana na
vitisho.
Ni jambo lisilo na shakka kuwa, msingi
na nguzo kuu ya nguvu ni wananchi na vikosi vya wananchi. Kabla ya
matukio ya mwaka 2011 katika ulimwengu wa Kiarabu ni Harakati ya
Mapambano ya Hizbullah ya Lebanon tu ndiyo iliyokuwa ikihesabiwa kuwa
nguvu yenye misingi ya wananchi.
Baada ya mwaka 2011 nchini Syria, Iraq
na Yemen nako kulisisitizwa suala la kurejea katika nguvu yenye msingi
na chimbuko la wananchi. Kuundwa vikosi vya kujitolea vya wananchi huko
Syria na Hashd al-Sha'bi huko Iraq sambamba na kuimarishwa Harakati ya
Wananchi ya Ansarullah ya Yemen ni miongoni mwa mambo yanayohesabiwa
kuwa dhihirisho la nguvu yenye misingi na chimbuko la wananchi.
Hata kama katika kipindi cha miaka
mitatu iliyopita kwa namna fulani kumekuweko na ushirikiano wa kiufundi
baina ya Ansarullah na vikosi vinavyofungamana na Chama cha Kongresi ya
Wananch kwa uongozi wa mwendazake Ali Abdallah Swaleh kwa ajili ya
kukabiliana na muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudia pamoja na
vikosi vinavyofungamana na Rais Abdu Rabbuh Mansour Hadi, rais
aliyejiuzulu na kuikimbia nchi, lakini kutokana na Ansraullah kupata
baraka za wananchi kutokana na kuwa kwake harakati ya wananchi,
haiwezekani kulilinganisha kundi hilo na makundi mengine ya Yemen.
Ni kwa msingi huo ndio maana njama na ukwamishaji mambo mbalimbali
uliofanywa na Ali Abdallah Swaleh katika kipindi cha miaka mitatu cha
kuwa pamoja na Ansarullah hasa katika nusu ya pili ya mwaka huu, haujawa
na natija yoyote ya maana kutokana na Ansarullah kupata uungaji mkono
wa wananchi. Kufeli njama za Ali Abdallah Swaleh siku mbili kabla ya
kufikia ukingoni maisha yake siku ya Jumatatu ni mfano wa wazi wa jambo
hilo.
Tunaweza kusema kuwa, kuibuka tukio
jipya la "Nguvu Yenye Chimbuko la Wananchi" hasa katika eneo la
Mashariki ya Kati katika miaka ijayo kunaweza kuunda nguvu tofauti
ambapo sifa muhimu ya nguvu hiyo ni kupunguza nafasi na mchango wa nguvu
kutoka nje kwa ajili ya kudhamini usalama.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: