JAFO MGENI RASMI KONGAMANO LA UWAJIBIKAJI KWA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA NCHINI DEC 5-6
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:48 AM
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za
Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jafo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi
katika kongamano la uwajibikaji kwa mamlaka za Serikali za mitaa
nchini linalotarajiwa kufanyika kuanzia kesho Desemba 5-6,2017 katika
hoteli ya Ramada iliyopo Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam.
Kongamano hilo linatarajiwa kuwa na
washiriki zaidi ya 120 ambao ni pamoja na Mameya/Wenyeviti wa
Halmashauri pamoja na Wakurugenzi Watendaji kutoka Halmashauri zaidi ya
120 kote nchini.
Akizungumza na wanahabari, Mkurugenzi
Mtendaji wa Shirika la WAJIBU (Wajibu Institute of Public
Accountability) Lodovick Utouh amesema kuwa tayarai maandalizi yote
yamekamilika huku washiriki mbalimbali tayari weanza kuwasili.
“Kongamano hili linatarajiwa kufunguliwa
na mgeni rasmi Waziri Mwenye dhamana Mh. Suleiman Jafo. Kongamano ili
pia hadi sasa tayari Mameya 50 na Wakurugenzi Watendaji 70
wamethibitisha kuhudhuria .
Mada mbalimbali zitawasilishwa na
kujadiliwa kwa kina na washiriki wa kongamano hili. Miongoni mwa mada
hizo ni pamoja na mkakati wa Serikali ya awamu ya tano wa utekelezaji
wa Sera yaa viwanda- ISDP, Mpnago wa pili wa Maendeleo 2016/17-2020/21
na mada zingine nyingi” alieleza Lodovick Utouh.
Utouh aliongeza kuwa, kongamano hilo
linatarajia kutoa taswira katika majadiliano na kufikia maazimio juu ya
mbinu zitakazotumika kufikia Tanzania ya uchumi wa Kati wa viwanda na
kuongeza uwajibikaji wa Serikali za Mitaa nchini katika usimamizi wa
rasilimali za Umma.
Taasisi hiyo ya WAJIBU ambayo ni taasisi
(think-tank organization) ya uwajibikaji wa umma iliyoanzishwa mwaka
2015 kwa lengo la kutengeneza mazingira ya kukuza uwajibikaji na Utawala
bora hapa nchini.
Aidha, kwa kutambua nafasi ya
kuongeza uwajibikaji na kuchangia maendeleo ya Taifa la Tanzania,
Taasisi ya WAJIBU kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Ujerumani
(GIZ) kupitia mradi wa (GFC) wamekuja na kongamano hilo lenye maudhui
“Ushiriki na Uwajibikaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa katika ujenzi
wa uchumi wa kati kupitia viwanda.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la WAJIBU
(Wajibu Institute of Public Accountability) Lodovick Utouh akizungumza
na wanahabari (Hawapo pichani ) wakati wa kutangaza kongamano hilo
linalotarajiwa kuanza kesho Desemba 5-6,2017.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: