Chama cha Wananchi (CUF) kimewaomba radhi wapiga kura wa Jimbo la Kinondoni kufuatia mbunge wa jimbo hilo Maulid Mtulia kujiuzulu Ubunge na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).
CUF YAWAOMBA RADHI WANACHAMA WAKE WA JIMBO LA KINONDONI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:44 AMChama cha Wananchi (CUF) kimewaomba radhi wapiga kura wa Jimbo la Kinondoni kufuatia mbunge wa jimbo hilo Maulid Mtulia kujiuzulu Ubunge na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza na Wanahabari leo jijini Dar
es Salaam, Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma CUF, Abdul
Kambaya, amesema chama hicho kinaomba radhi kutokana na kuwaaminisha
wapiga kura kwamba Mtulia ni mtu makini mwenye uwezo wa kusimamia Sera
za CUF na maendeleo ya Kinondoni.
“CUF haikutarajia kuingia kwenye
uchaguzi mdogo kwa jimbo la Kinondoni kabla ya uchaguzi wa 2020 labda
kama ingetokea kifo. Tunaomba radhi kwa kuwa tunaamini katika kurudia
uchaguzi zitatumika fedha za umma wakati kwa hali tuliyo nayo fedha hizo
zingeweza kuelekezwa kwenye shughuli za miradi ya maendeleo. Sababu za
Mtulia kujiudhuru ni za msingi kwake lakini kwa upande wetu tunaziona
hazina mashiko,” amesema
Kambaya amesema CUF inajiandaa kushiriki
katika uchaguzi wa marudio ili kutetea jimbo la Kinondoni na kwamba
itahakikisha inateua Mgombea makini na muadilifu atakayeleta ushindi kwa
chama hicho.
Na Regina Mkonde
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: