NYALANMDU AUNGANA NA VIONGOZI WA CHADEMA, MAZISHI YA MCHUNGAJI LOOKA MUSHI, ALIYEKUWA MKUU WA JIMBO WA CHAMA HICHO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:16 AM
Waziri Mstaafu wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu, (kushoto), akiungana na
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mhe Freeman Mbowe (Watatu kushoto) na viongozi wengine wa chama hicho, kwenye mazishi ya
Mkuu wa jimbo mstaafu wa chama hicho, marehemu Looka Mushi,
yaliyofanyika jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro, Novemba 17,
2017. Nyalandu ambaye pia alikuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, alijivua
vyeo vyote ikiwemo uanachama wa CCM na sasa anasubiriwa kujiunga rasmi
na CHADEMA.
Mheshimiwa Mbowe, akiweka shada la mauwa kwenye kaburi la marehemu, Looka Mushi,
yaliyofanyika jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro, Novemba 17,
2017.
Mheshimiwa Mbowe, akitoa heshima mbele ya kaburi la marehemu Mushi wakati wa mazishi yake.
Mheshimiwa Nyalandu akiwa na Mbunge wa
Arusha Mjini, Mhe. Godbless Lema wakitoa heshima za mwisho mbele ya
jeneza lenye mwili wa marehemu.
Mheshimiwa Mbowe, akitoa heshima zake mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Mushi.
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa,Mhe Freeman
A. Mbowe (Wapili kushoto) akiwa na Mbunge wa Arusha mjini,Mhe
Godbless Lema , Waziri Mstaafu wa Mali Asili na Utalii, Lazaro
Nyalandu, Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi,Uenezi na Mambo ya Nje
CHADEMA, John Mrema, kabla ya kuelekea kwenye msiba wa Mkuu wa jimbo
mstaafu, Mchungaji Looka Mushi huko jimboni Hai, Novemba 17/11/2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: