KUULIWA WAISLAMU MSIKITINI KATIKA SAMBULIO LA BOMU LA KUJITOA MHANGA NCHINI NIGERIA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:27 AM
Watu wasiopungua 50 wameaga dunia katika mlipuko wa bomu uliotokea msikitini kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Othman Abubakar Msemaji wa polisi
ya Nigeria ametangaza kuwa shambulio hilo la kujitolea mhanga dhidi ya
msikiti katika mji wa Mubi jimboni Adamawa lilifanywa wakati waumini
walipokuwa katika Sala ya Alfajiri. Kundi la kigaidi la Boko Haram
limetangaza kuhusika na shambulio hilo.
Hii ni mara ya kwanza kutokea tukio kama
hilo la kigaidi tangu kukombolewa mji wa Mubi kutoka mikononi mwa kundi
la kigaidi la Boko Haram mwaka 2014. Hujuma na mashambulizi ya kigaidi
ya Boko Haram hadi sasa yamesababisha kuuliwa watu zaidi ya elfu 20 huko
Nigeria. Kundi hilo linaendeleza hujuma zake hizo za kigaidi khususan
dhidi ya Waislamu wa Nigeria; huku kwa muda sasa jeshi la nchi hiyo
likidai kuwa linafanya juhudi za kuliangamiza.
Udhaifu wa jeshi la Nigeria na kushindwa
kwake kukabiliana na makundi ya kigaidi kumeyaandalia fursa makundi
hayo ya kuendeleza harakati zao likiwemo kundi la Boko Haram. Kuna
ishara zinazoonyesha kuwa baadhi ya nchi za Magharibi na utawala wa
Kizayuni zinaliunga mkono nyuma ya pazia kundi la kigaidi la Boko Haram
nchini Nigeria ili kuendelea kudhamini maslahi yao ya kisiasa na
kiuchumi kwa kulipatia kundi hilo misaada ya silaha na zana za kijeshi
kisirisiri ili kuliimarisha.
Jeshi la Nigeria huko nyuma liliwahi
kunasa silaha elfu 10 yakiwemo makombora aina ya M-302 yaliyoundwa
Israel ambayo yana uwezo wa kulenga umbali wa kilomita 200. Silaha hizo
zilinaswa katika kambi ya Boko Haram katika msitu wa Sambisa kaskazini
mashariki mwa nchi. Uchunguzi uliofanywa na maafisa usalama kuhusiana na
suala hilo unaonyesha kuwa silaha hizo zilitumwa moja kwa moja kwa Boko
Haram kutoka Israel. Aidha mkono wa Israel unashuhudiwa katika
mashinikizo yanayozidi kuwaandama Waislamu wa nchi hiyo. Viongozi wa
utawala ghasibu wa Kizayuni ambao wamegonga mwamba katika siasa zao
katika eneo hili la Mashariki ya Kati; hivi sasa wanatafuta eneo jingine
barani Afrika la kuwa na ushawishi ambapo Nigeria inaonekana kuwa
chaguo lao zuri kutokana kuwa na makabila mengi na nafasi nzuri ya
kiuchumi na kisiasa.
Sheikh Adam Soho, mwanachama
mwandamizi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria anasema kuwa: Serikali ya
Nigeria iko chini ya ushawishi wa serikali za Saudi Arabia, Marekani na
utawala wa Kizayuni na pande zote hizo zinaendesha njama dhidi ya
Waislamu khususan wa madhehebu ya Shia nchini Nigeria.
Katika
upande wa kiuchumi, Nigeria ni nchi yenye umuhimu; ni nchi ambayo ina
jamii ya kizazi cha vijana na utajiri mkubwa wa mafuta, ambayo siku zote
imekuwa ikikodolewa jicho la tamaa na madola ya kikoloni. Kwa msingi
huo kuwepo mivutano ya kisiasa na kiusalama kunayaandalia fursa madola
hayo ya kutimiza malengo yao nchini humo. Aidha nchi nyingi za
Magharibi zimekuwa zikizungumzia suala la kuisaidia Nigeria katika vita
dhidi ya Boko Haram, na si tu kuwa kivitendo nchi hizo hazijatoa msaada
wowote kwa Nigeria, bali zimekuwa zikishadidisha tu hujuma za kundi
hilo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: