MOHAMMADI- GOLPAYEGANI: MAADUI HAWAWEZI KULIKATISHA TAMAA TAIFA LA IRAN KWA KUFANYA MAUAJI

Mkuu wa ofisi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, hatua ya maadui ya kufanya mauaji katu haiwezi kulikatisha tamaa taifa la Iran.
Hujjatul Islam Walmuslmiin Muhammad Muhammadi-Golpayegani, amebainisha kuwa, sababu ya mashambulio ya juzi ya kigaidi hapa mjini Tehran ni safari ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani nchini Saudi Arabia.
Akizungumza katika shughuli ya kuiaga miili ya mashahidi wa mashambulio ya kigaidi ya siku ya Jumatano hapa mjini Tehran, mkuu wa ofisi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, katika safari ya hivi karibuni ya Trump nchini Saudia kuliratibiwa mipango ya kutoa pigo dhidi ya Iran.
Muhammad Muhammadi Golpeygani, Mkuu wa ofisi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
Aidha Hujjal Islam Walmuslimiin Muhammad Muhammadi Golpeygani alisoma ujumbe wa rambirambi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa mnasaba wa mashambulizi ya kigaidi yaliyofanyika siku chache zilizopita mjini Tehran akisisitiza kuwa, jinai hiyo haiwezi kutia doa katika irada na azma ya taifa la Iran.
Akizungumza katika hafla hiyo ya kuaga miili mitoharifu ya mashahidi wa mashambulio hayo ya kigaidi, Ali Larijani, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mashambulio hayo ya kigaidi yameonyesha jinsi magaidi walivyojikita zaidi katika kulenga mhimili mkuu wa mfumo wa utawala wa kidini nchini Iran wenye ridhaa ya wananchi.

0 comments: