MFALME WA MOROCCO AKOSA KUHUDHURIA MKUTANO WA ECOWAS KWA AJILI YA NETANYAHU

Mfalme Muhammad wa Sita wa Morocco amekosa kuhudhuria mkutano wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Magharibi mwa Afrika (ECOWAS) unaofanyika leo nchini Liberia kwa kuwa unahudhuriwa na Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Benjamin Netanyahu.
Awali mfalme huyo alikuwa amekubali mwaliko wa kushiriki kongamano hilo lakini alipofahamishwa kuwa litahudhuriwa na Netanyahu, akatangaza kughairi msimamo huo.
Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Morocco imesema Mfalme Muhammad wa Sita wa Morocco amefuta uamuzi wake wa kuhudhuria kikao hicho cha kikanda kwa kuwa kinafanyika chini ya mazingira ya taharuki, mikwaruzano na mkanganyo.
Baadhi ya viongozi wa nchi wanachama wa ECOWAS
Ifahamike kuwa Morocco sawa na nchi nyingi za Kiarabu haina uhusiano wa kidiplomiasia na utawala haramu wa Israel.
Nchi 15 wanachama wa ECOWAS zinahudhuria kongamano hilo eti la kuimarisha uhusiano wa kibiashara na Israel, zikiwemo Mali na Niger ambazo pia hazina uhusiano wa kidiplomasia na Tel Aviv.
Licha ya kuwa nchi nyingi za Kiarabu zimetangaza kutokuwa na uhusiano na utawala pandikizi wa Israel, lakini duru za habari zinaashiria kuwa aghalabu yazo zina uhusiano wa kisiri na Tel Aviv.

0 comments: