Hatimaye serikali ya Côte d’Ivoire yakubaliana na askari waasi

Viongozi wa serikali ya Côte d’Ivoire wametangaza kufikiwa makubaliano na askari waasi wa nchi hiyo.
Alain Richard Donwahi, Waziri wa Ulinzi wa Côte d’Ivoire amesema kuwa, tayari yamefikiwa makubaliano na askari hao waasi nchini. Hii ni katika hali ambayo viongozi wa askari hao wametangaza habari ya kutofikiwa makubaliano na serikali ya taifa hilo Uasi wa askari nchini Côte d’Ivoire  uliibuka siku ya Jumapili iliyopita kwa kufanya vurugu katika mji wa kibiashara wa Abidjan na Bouaké.
Alain Richard Donwahi, Waziri wa Ulinzi wa Côte d’Ivoire
Mapema jana watu sita waliripotiwa kujeruhiwa kwa risasi huko Bouaké, ambao bado uko mikononi mwa wanajeshi hao walioasi nchini Kodivaa. Shirika la habari la Ufaransa liliripoti kuwa, wanajeshi waasi waliwafyatulia risasi watu katika mji wa pili wa Ivory Coast ulioko mikononi mwa wanajeshi hao waaasi katikati ya nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mwanamke mmoja na wanaume watano wamejeruhiwa kwa risasi na kuwahishwa hospitalini huko Bouaké.
Askari waasi Ivory Coast
Kabla ya hapo pia, Baraza la Usalama wa Taifa la Ivory Coast lilifanya kikao cha dharura kufuatia kushadidi fujo zilizosababishwa na uasi huo wa wanajeshi.

0 comments: