19 WAUAWA KATIKA HUJUMA YA KIGAIDI MANCHESTER, UINGEREZA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:58 AM
Watu wasiopungua 19 wameuawa katika mji wa
Manchester nchini Uingereza kufuatia mlipuko mkubwa unaoshukiwa kuwa
hujuma ya kigaidi.
Watu wengine zaidi ya 50 wanaripotiwa kujeruhiwa katika tukio
hilo la Jumatatu usiku katika ukumbi wa Manchester Arena ambapo vijana
wengi walikuwa wamekusanyika kutumbuizwa na muimbaji kutoka Marekani.
Walioshuhudia tukio hilo wanasema walisikia sauti ya mlipuko mkubwa
baada ya muimbaji Ariana Grande, raia wa Marekani, kumaliza muziki wake.
Mkuu wa Polisi Manchester Ian Hopkins amethibitisha kuuawa watu hao
19 huku akithibtisha kuwa tukio hilo kwa sasa linatazamwa kama hujuma ya
kigaidi.
Baadhi ya duru za usalama zinadokeza kuwa hujuma hiyo imetekelezwa na mlipuaji aliyekuwa amejifunga mabomu mwilini.
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ametoa taarifa na kusema uchunguzi unafanyika kubaini iwapo hujuma hiyo ilikuwa ya kigaidi.
Alhamisi iliyopita Mkuu wa Idara ya Kupambana an Ugaidi katika Baraza
la Usalama la Umoja wa Mataifa Jean-Paul Laborde alikuwa ameonya kuwa
kuna wimbi la magaidi wa ISIS wanaorejea Ulaya baada ya kushindwa katika
vita huko Iraq na Syria.
Aidha mapema mwezi huu mashirika ya kijasusi ya Uingereza yalionya
kuwa raia 350 wa nchi hiyo ambao ni magaidi wanachama wa kundi la
kigaidi la ISIS wamerejea nchini humo kutoka Syria na sasa ni tishio
kubwa kwa usalama.
Maafisa wa usalama wanasema magaidi hao sugu ambao waliondoka
Uingereza na kujiunga na kundi hilo la wakufurishaji wamekuwa
wakitarajiwa kurejea nyumbani kwani ISIS imekuwa ikipata pigo Syria na
Iraq na hivyo kupoteza ardhi ambazo ilikuwa imezikalia kwa mabavu.
Mashirika ya usalama Uingereza yanasema ni vigumu kufuatilia kila
gaidi aliyerejea kwani idadi yao ni kubwa na wanarejea kwa mpigo.
Hujuma ya Manchester imejiri pamoja na kuwa usalama umeimarisha
Uingereza baada ya kujiri shambulizi nje ya jengo la bunge mjini London
hivi karibuni ambapo watu wanne walipoteza maisha wakati gaidi mmoja
aliendesha gari kiholela na kuwagonga wapita njia huku akimdunga kisu
polisi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: