RAIS WA TUNISIA: IRAN NDIYO TEGEMEO PEKEE KWA AJILI YA KUKABILIANA NA ISRAEL

Rais Beji Caid Essebsi wa Tunisia amesema kuwa Iran ndio tegemeo pekee kwa ajili ya kukabiliana na Israel.
Rais wa Tunisia ameyasema hayo katika mazungumzo yake na Waziri wa Utamaduni wa Iran aliyeko nchini humo na kuongeza kuwa, adui mkubwa zaidi wa Iran katika eneo la Mashariki ya Kati ni utawala wa Kizayuni wa Israel na kwamba anatarajia nchi zote za Kiislamu na Kiarabu zitakuwa bega kwa bega na Iran katika suala hilo.
Beji Caid Essebsi amesema utawala wa Kizayuni na washirika wake wanafanya jitihada za kuitenga Jamhuri ya Kiislamu lakini njama hizo zimegonga mwamba. Amesisitiza kuwa, Iran ni nchi kubwa na yenye utamaduni tajiri na kwa msingi huo inapaswa kutekeleza majukumu yake katika eneo la Mashariki ya Kati. 
Rais wa Tunisia, Beji Caid Essebsi 
Rais wa Tunisia amesema kuwa nchi yake haitaathirika na misimamo ya nchi nyingine katika uhusiano wake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. 
Kwa upande wake Waziri wa Utamaduni ya Miongozo ya Kiislamu wa Iran, Ridha Salehi Amiri amesifu uhusiano mzuri wa kiutamaduni, kiuchumi na kibiashara wa Iran na Tunisia.
Ameashiria hali ya sasa ya Mashariki ya Kati na kusema: Hali ya eneo hilo imebadilika sana baada ya matukio ya Iraq na Syria na kuongeza kuwa: Kama si mapambano ya Iran dhidi ya magaidi waliovamia nchi hizo hii leo magaidi wangekuwa katika miji ya Baghdad na Damascus na kirusi hicho kingezikumba nchi nyingine za Waislamu.  

0 comments: