MAKAMU WA RAIS SAMIA, AJIONEA UTIRIRISHAJI HAFIFU WA MAJI KWENYE MTO WA RUAHA MKUU
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:28 PM
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan
ameuahidi uongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na wa Mkoa wa Iringa kuwa
Serikali italifanyia kazi tatizo la ubovu wa barabara kutoka Iringa
mjini Hadi katika hifadhi hiyo ili kuongeza idadi ya watalii katika
Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan
ametoa kauli hiyo katika mkutano wake na Viongozi wa Hifadhi hiyo na wa
mkoa wa Iringa baada ya kufanya ziara fupi katika hifadhi hiyo pamoja na
kujionea utiririshaji hafifu wa maji katika Mto Ruaha uliosababishwa na
shughuli za kibinadamu hasa kilimo.
Makamu
wa Rais amesema serikali itahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa awamu
kwa kiwango cha lami kama hatua ya kuongeza maradufu idadi ya watalii
katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ambapo kutokana na ubovu wa barabara
kuelekea hifadhi hapo idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi hiyo
imeendelea kupungua kila uchao.
Kuhusu
vitendo vya ujangili hifadhi hapo, Makamu wa Rais ameuagiza uongozi wa
hifadhi hiyo kushirikiana na wananchi wanaozunguka hifadhi hiyo ili
kuwabaini majangili na kuwachukulia hatua ili kukomesha vitendo hivyo.
Amesema
idadi kubwa ya majangili wanatoka miongoni mwa jamii zinazozunguka
Hifadhi ya Taifa ya Ruaha hivyo wananchi wakishirikishwa kikamilifu
katika kutoka taarifa za siri majangili wengi watakamatwa na
kuwajibishwa.
Awali
akitoa taarifa kwa Makamu wa Rais, Kuhusu utendaji kazi wa Hifadhi
hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ALLAN KIJAZI
aliiomba serikali isaidie kulinusuru bonde la Usangu ili liweze
kurejesha mtitiriko wa maji kwa ajili ya matumizi ya hifadhi hiyo na
kumaliza mgogoro wa mpaka kati ya hifadhi na wananchi ambao umedumu kwa
muda mrefu bila suluhu kupatikana.
Amesema
mapaka sasa TANAPA imeshatumia zaidi ya shilingi bilioni SABA kwa ajili
ya kulipa fidia wananchi na gharama nyingine ili kunusuru bonde hilo
lakini bado kuna changamoto ambazo zinaathiri usimamizi wa eneo hilo na
zinahitaji maamuzi ya serikali.
Mkurugenzi
huyo Mkuu wa TANAPA pia amepongeza msukumo wa dhati wa serikali ya
awamu ya Tano katika kusimamia hifadhi ya mazingira na maliasili kwani
jitihada hizo zitasaidia kuboresha mazingira na viumbe hai kwa ajili ya
vizazi vya sasa na vijavyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: