WANAMTANDAO WA DAWA ZA KULEVYA WABUNIFU WA KILA NJIA ZA KUSAMBAZA –KAMISHINA SIANGA

Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Siangaakizungumza katika hafla ya timu ya Serengeti Boys chini ya miaka 17 kutembelea kituo cha watu waliodhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani jana.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum akizungumza katika hafla Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu walioadhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani juu ya viongozi wa dini walivyo mstari wa mbele katika kupambana na dawa za kulevya.
Rais wa TFF, Jamal Malizi akizungumza katika hafla Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu waliaodhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Mkurugenzi wa Sober House, Al-Karim Banji akizungumza katika hafla Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu waliodhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani. (Picha zote na Emmanuel Massaka Globu ya Jamii).
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum (kushoto) akipeana mkono wa shukrani na Rais wa TFF, Jamal Malizi katika hafla Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu walioadhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Siangaakisalimina na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum katika hafla ya Timu ya Serengeti Boys chini ya miaka 17 kutembelea kituo cha watu waliodhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Siangaakimkabidhi cheti , Rais wa TFF, Jamal Malizi katika hafla Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu walioadhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Sianga akimkabidhi cheti , Mwakilishi Michuzi Media Group,Emmanuel Massaka katika hafla ya Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu waliodhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Sianga akiwa katika picha ya pamoja wachezaji wa Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) baada timu hiyo kutembelea kituo cha Sober House jana (Picha zote na Emmanuel Massaka Globu ya Jamii).
.Kocha Mkuu wa Serengeti Boys, Kim Poulsen (kushoto)akimkabidhi mipira na jezi Mkurugenzi wa Sober House, Al-Karim Banji katika katika hafla ya Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu waliodhirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober Hoouse)kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Wadau mbalimbali

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Kamishina wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya nchini,Rogers Sianga amesema kuwa vita ya kupambana na dawa za kulevya ni kubwa kutokana na kila siku watu wanabuni njia mpya.

Vita ya dawa za kulevya sio lelema kutokana na kuwa watu ambao wana mbinu nyingi za kufanya hivyo, lakini watakamatwa wote na hatuingii kichwa kichwa katika kufanya kazi hiyo.

Akizungumza jana katika hafla ya Timu ya Vijana chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kutembelea kituo cha watu walioathirika na matumizi ya dawa za kulevya (Sober House) kilichopo Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.

“Watu watano tumewakamta na mmojawapo aliyekuwa anasambaza dawa za kulevya Tanzania Bara na Zanzibar na jumla zaidi watu 11000 wamekamatwa ’’amesema Sianga.

Sianga amesema mtandao wote unaofanya biashara ya dawa za kulevya wameukamata, na wanaendelea kupokea taarifa mbalimbali za kuweza kutokomeza mtandao wa kuingiza dawa hizo.

Amesema wanatumia njia tatu katika kupata taarifa za watu wanaofanya biashara hiyo moja ni taarifa za watu za moja kwa moja ya pili utafiti pamoja wananchi.

Aidha amesema kuwa watashirikiana na watu wa sober house katika mihadhara ya kuelimisha juu madhara ya dawa za kulevya kwa wale waliotumia na wamepona kwa sasa.

Sianga amesema anaona furaha kuona viongozi wa dini wako mstari wa mbele na kufanya atembee kifua mbele.

Kamishina huyo ametoa msaada wa Ngamizi Moja ‘Komputa’kuajili kuendeshea kazi katika kituo hicho, Mwenyekiti wa Chama cha Mpira Miguu Mkoa wa Pwani Hassan Hassanoo ametoa Ekari moja pamoja na Rais wa TFF, Jamal Malizi ametoa fedha taslimu Sh.Milioni 1.2 sambamba na mipira na jezi.
Mkurugezi wa Sober House , Al-Karim Banji amesema kuwa changamoto iliyokuwa mbele yake katika kituo hicho ni kukosa eneo ambalo linaweza kukidhi mahitaji kwa wanaume na wanawake.

Amesema kituo kinapokea wanaume tu wakati wapo wanawake walioathirika na hawajaweza kupata msaada huo.

0 comments: