TUNDU LISSU ASHINDA KWA KISHINDO URAIS TLS


HATIMAYE mkutano mkuu wa Chama cha Mawakili Tanganyika, (TLS), umemchagua mwanasheria machachari nchini, Tundu Lissu, kuwa Rais wa chama hicho.
Katika uchaguzi huo uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa. (AICC), jijini Arusha  Machi 18, 2017, Lissu ambaye pia ni mwanasheria mkuu wa CHADEMA, amejinyakulia jumla ya kura 1,411 sawa na asilimia 88% ya kura zote 1,682, zilizopigwa.
Mbali na Lissu wagombea wengine waliokuwa wakichuana na Lissu ni Victoria Mandari,Francis Stolla  na Godwin Mwapongo.
Aidha wakili Godwin Ngwilimi ambaye aliwahi kuwa Mwanasheria wa TANESCO amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais na Magai kuwa Mweka hazina.
Aidha imewachagua mawakili  saba kuwa wajumbe wa Baraza la TLS ambao ni 
Jeremiah Motebesya,Gida Lambaji
,Hussein Mtembwa
,Aisha Sinda, Steven Axweso,David Shilatu
na Daniel  Bushele.
Uchaguzi wa TLS mwaka huu umetupa mafunzo mengi kwa wale tunaopenda kujifunza kuwa wànasheria ni watu wenye misimamo  yao na siyo kazi rahisi kuwayumbisha kwasababu wanafahamu sheria na haki zao.
Pia TLS imejikuta ikipata umaarufu na kujulikana kwa watu waliokuwa hawaifahamu TLS  kutokana Rais John Magufuli katika moja ya hotuba yake kuinyoshea kidole TLS wakati tayari Kamati ya uchaguzi ilikuwa imeishapitisha majina ya wagombea ambao wamegiwa kura leo,Waziri wa Katiba na Sheria Dk.Harrisso Mwakyembe kutoa tamko lq kutishia kuifuta TLS kwasababu inai ngiza siasa,baadhi ya wafuasi wa CCM nao waliibuka mitandaoni wakimtuhumu Lissu azuiwe kugombea TLS maana ataleta siasa TLS .
Na wale wafuasi wa Chadema na makundi mengine yaliyokuwa yakimuunga mkono Lissu yalimkingia kifua Lissu wakisema anafaa na kwamba hata baadhi ya wagombea TLS ni wanachama CCM.
Aidha kitendo cha mawakili wawili,Onesmo Mpenzile na Godfrey Wasonga kufungua kesi za kuzuia uchaguzi wa TLS usifanyike leo zilizokuwa zimefunguliwa katika Mahakama Kuu Dodoma,Dar es Salaam ambazo zote hizo mbili mahakama ilizitupila mbali nazo zilisaidia kuitangaza TLS bila gharama za kulipia matangazo.
Lissu akiwa na mkewe

0 comments: