TANESCO YATOA TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA UMEME MAENEO YA KIBAMBA, MBEZI NA KIMARA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:05 AM
SHIRIKA la
Umeme Tanzania TANESCO linawataarifu wateja wake wa maeneo ya Kimara, Mbezi
yote na Kibamba yote kuwa, Kumetokea hitilafu katika Laini inayosambaza umeme
katika maeneo hayo (NORDIC 1 &2) tangu jana Tarehe 18/03/2017 majira ya saa
nane mchana Kutokana na Mvua kubwa iliyonyesha na kuathiri miundombinu ya umeme
katika maeneo hayo na hivyo kupelekea kukosekana kwa huduma ya umeme kwa wateja
wa maeneo hayo.
HATUA
ZILIZOCHUKULIWA
Mafundi
walichukua hatua za haraka kurejesha umeme tangu jana na kufanikiwa kurejesha
huduma katika maeneo machache. Ili kurahisisha Kazi ya kubaini Hitilafu hiyo,
Mafundi walilazimika kuzima laini zote mbili tena kwa siku ya leo na mpaka Hivi
sasa mafundi wetu bado wako mtaani wakiendelea na jitihada za kurejesha umeme
katika hali ya kawaida kwa maeneo yote yanayohudumiwa na laini hizi mapema
iwezekanavyo.
Uongozi wa
Shirika unaomba radhi kwa usumbufu wowote ule unaojitokeza.
Imetolewa
na:
OFISI YA
UHUSIANO TANESCO MAKAO MAKUU
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: