RISASI 360 ZAKAMATWA NA WATUHUMIWA SITA KUFIKISHWA MAHAKAMANI-KIGOMA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:22 PM
Akibainisha hayo juzi ofisini kwakwe mbele ya mwandishi wa blog ya ujijirahaa Mkoani kigoma Ujiji, Kamanda wa Polisi, Ferdinand Mtui alieleza kuwa, uelewa wa wananchi juu ya kubaini viashiria vya wahalifu ni matunda ya kupatikana kwa silaha hizo sanjari na watuhumiwa wa matukio hayo.
“ndugu mwandishi matukio haya saba ni ya wiki moja tangu uanze mwezi huu, ambapo silaha za moto mbalimbali zimekamatwa kama gobore 8, mark four 1, risasi 319, huku risasi 156 za silaha aina ya SMG/SAR/ RISASI 10 silaha ya G3 na Short gun sambamba na gololi 44 za gobore” alifafanua DCP Mtui.
Aliyataja majina ya watuhumiwa waliokutwa na tuhuma hizo ni pamoja na Josephat Kanumwa(45) Gerishoni Bilatata(36), Kisore William(31), Japhet Mkuyu(40) na Juma Ndiyunguye(35) huku wengine wakifanikiwa kutoroka katika matukio ya uwindaji haramu, ambapo watafikishwa Mahakamani hivi punde baada ya uchakataji wa upelelezi kukamilika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: