RC-MWANRI ATAKA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA KANDA YA MAGHARIBI WAWE WABUNIFU
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:34 AM
NA MAGNAETH MAGOSSO,KIGOMAN
MWENYEKITI wa
Baraza la uwezeshaji Uchumi kwa wananchi Kanda Magharibi ambaye pia ni Mkuu
wa Mkoa wa
Tabora Agrey Mwanri amewataka viongozi
wa Mikoa na wilaya wawe wabunifu wa fursa pamoja na kusimamia mifuko ya uwezeshaji wa kiuchumi
kwa wananchi ,ili kupunguza umaskini
kuanzia ngazi ya familia na mkoa kwa ujumla.
Pia amesema hatapitisha bajeti ya mwaka wa fedha katika
halmashauri ya mkoa wake endapo bajeti
haitaonyesha kutengwa kwa 5% ya fedha za vijana na 5% ya wanawake
kwa ajili ya kuwakopesha kupitia vikundi vyao kwa lengo la kupunguza kero ya kipato duni.
Aliyasema hayo katika ufunguzi wa
mafunzo ya siku tatu iliyosimamiwa na Baraza la Taifa la uwezeshaji wa kiuchumi
wa wananchi alieleza kuwa, kitendo cha baadhi ya viongozi wa mikoa ,wilaya na wakurugenzi wa halmashauri kuwa
miongoni mwa walalamikaji wa kero
mbalimbali zinazowakabili wananchi ni
kutojitambua nafasi zao kwa jamii .
Alifafanua
kuwa,kupitia fursa za mikoa yao ni chachu ya kubaini masoko ya rasilimali zilizopo katika mkoa
wake na kupitia tarifa za wadau wa sekta mbalimbali za kiuchumi atajua eneo la
kuwawezesha wakulima,wajasiliamali na wafanyabiashara kunufaika na fursa za
hapo.
“viongozi waongoze njia kwa kubainisha mahitaji ya masoko mbalimbali ya kibiashara ,wasimamie mifuko ya uwezeshaji
wa wananchi,serikali inajitihada kubwa ya kuwa na uchumi wa viwanda kila
kiongozi wa serikali atawambue uwepo wake” alisisitiza Mwanri.
Kwa upande wa Katibu Mtendaji wa
baraza hilo Beng`I Issa alisema lengo
kubwa ni viongozi kutambua majukumu yao kwa kuwawezesha kiuchumi wananchi kupitia mifuko ya uwezeshaji katika
vikundi vya vijana,wanawake,wajasiliamali na wafanyabiashara kwa ujumla.
Issa alieleza kuwa,washirikishe
wadau wa sekta mbalimbali za maendeleo ,ili mifuko ya fedha za umma ziwafikie
walengwa kwa kukopeshwa kupitia vikundi ili,kuondoa kero ya umaskini kwa wananchi
waliowengi na kupitia mafunzo hayo mikoa ya kigoma ,katavi,kagera na Tabora ni
wanufaika a mafunzo hayo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: