Ni wajasiliamali wa uhakika.
RC KIGOMA ATAKA WAKURUGENZI NA WAKUU WA WILAYA MIZIGO WAONDOKE KIGOMA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:14 AM
Na Magreth Magosso,Kigoma
MKUU wa Mkoa wa Kigoma Emanuel Maganga amewataka
wakurugenzi na wakuu wa wilaya wasiowajibika katika kuwaletea wananchi
maendeleo wachie nafasi hizo ili wateuliwe wenye uwezo wa kutatua
changamoto zinazowakabili wakazi wa Kigoma .
Pia ashangazwa na baadhi ya viongozi hao kushindwa kuandaa
Mpango wa wanufaika wa ujio wa fedha za rais john magufuli ya
sh.milioni hamsini kwa kila kijiji na maeneo ya viwanda ilihali kila
wilaya Ina nishati ya umeme.
Maganga alisema hayo jana kigoma Ujiji katika kikao cha kamati ya
ushauri Mkoa uliolenga kupitia mapendekezo ya bajeti ya mwaka wa fedha
wa 2017/18 na kusema kuwa, viongozi hao ni wasomi, vijana lakini Elimu
yao haiwanufaishi wananchi katika sekta mbalimbali hasa kilimo ambapo
wananchi hawapati Huduma ya kilimo cha kisasa.
,,Hakuna kiongozi mgeni, fanyeni kazi ajabu miongoni kwa
viongozi mnalima hekari hamsini kwa kutumia trekta lakini hamshirikishi
wananchi watumie zana za kisasa katika sekta ya kilimo,, alifafanua mkuu
wa Mkoa huo.
Alieleza kuwa, kitendo cha kushindwa kuandaa maeneo ya
viwanda na wanufaika wa fedha za rais ni dalili za ubadhilifu wa fedha
na wananchi lengwa kutokunufaika na mamilioni ya rais Magufuli.
Aisha alisema watendaji wengi wa serikali wana Tania ya
kuigiza Maisha ya wananchi wenye hitaji la kusaidiwa na serikali yao,
lakini changamoto zinazoshindwa kutoweka kutokana na sintofafamu ya
watendaji husika kutokuwajibika ipasavyo.
Alisema halmashauri za mkoani hapo zinakabiliwa na kero ya
asilimia 5%ya kuwakopesha vijana na 5% ya kuwakopesha wanawake,kimsingi
wanawake wa kigoma
Ni wajasiliamali wa uhakika.
Ni wajasiliamali wa uhakika.
Katika kikao hicho kiasi cha fedha sh.bilioni 248.29
zimekadiriwa kutumika katika mwaka 2017/18 kwa ajili ya matumizi ya
kawaida na Miradi ya maendeleo ya wananchi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: