RAIS MAGUFULI "AMTUMBUA" KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU, ULEDI ABASS MUSSA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 8:44 PM
RAIS John Pombe Magufuli, ametengua
uteuzi wa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, (Bunge), Bw. Uledi Abass Mussa kuanzia jana
Machi 15, 2017.
Taarifa ya Ikulu iliyotolewa jana kwa
vyombo vya habari na kusainiwa na Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya
Rais, Ikulu, Gerson Msigwa ikimnukuu Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imesema,
sambamba na hatua hiyo Katibu Mkuu Uledi pia amesimamishwa kazi ili kupisha
uchunguzi wa tuhuma dhidi yake.
Taarifa hiyo imezitaja tuhuma hizo kuwa
ni kushindwa kwa Bw. Uledi kusimamia taratibu zinazotakiwa katika kushughulikia
taratibu za uwekezaji.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: