NYUMBA KADHAA ZILIZOJENGWA JIRANI NA RELI ZABOMOLEWA HUKO BUGURUNI JIJINI DAR ES SALAAM
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:33 AM
NA
K-VIS BLOG
NYUMBA
kadhaa zilizojengwa ndani ya mita 30 kutoka reli ya kati eneo la Buguruni
jijini Dar es Salaam, zimebomolewa mapema leo alfajiri Machi 11, 2017.
Mashuhuda
wanasema, mapema alfajiri tingatinga likisimamiwa na askari wa kikosi cha
kutuliza ghasia, walifanya zoezi hilo la kubomoa nyumba hizo huku wenye nyumba
na wapangaji wakihamisha mali zao.
Taarifa
zinasema wenye nyumba hizo waliwekewa alama za X zikimaanisha nyumba hizo
hazikustahili kujengwa kwenye eneo hilo na kwamba wamiliki wake walitakiwa
kuzibomoa.
Pichani
ni jinsi zoezi hilo lilivyokuwa likiendela.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: