MBUNGE TUNDU LISSU AKAMATWA NA POLISI AKITOKA MAHAKAMANI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:14 AM
Jeshi la
Polisi nchini linamshikilia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu
baada ya kuachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.Lissu
aliachiwa leo asubuhi na Hakimu Mkuu Mkazi, Huruma Shahidi baada ya
upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili Paul Kadushi kuwasilisha hati ya
kuondoa shtaka hilo.Kadushi aliwasilisha hati hiyo chini ya kifungua
namba91 (1) cha makosa ya jinai akionyesha DPP hana haja ya kuendelea na
kesi, mahakama ikaridhia na kumuachia.
Muda
mfupi baada ya kuachiwa na kutoka nje ya mahakama alikamatwa tena na
askari waliokuwapo mahakamani hapo na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi.
Lissu
alikuwa anashtakiwa kwamba Januari 11, mwaka huu katika kampeni za
uchaguzi jimbo la Dimani aliwashawishi watu wasiridhike na wawe na nia
ovu dhidi ya utawala.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: