LEMA, WEMA SEPETU WAHUTUBIA MAELFU YA WANANCHI JIJINI ARUSHA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:27 AM
Mbunge wa Arusha Mjini, (CHADEMA),
Godbles Lema, (kushoto),akiwa na Miss Tanzania wa zamani, Wema Sepetu
kwenye mkutano wake wa kwanza wa hadhara leo Machi 10, 2017 jijini
Arusha tangu aachiliwe kwa dhamana kufuatia kesi ya uchochezi
inayomkabili.
Lema ambaye alipewa dhamana mapema wiki
hii baada ya kukaa rumande kwa muda mrefu, alisema, ataendelea kutetea
demokrasia bila woga, kauli ambayo iliungwa mkono na Wema Sepetu ambaye
pia ni msanii maarufu wa filamu, ambaye naye alisema, yuko bega kwa bega
na Lema katika kutetea demokrasia ya nchi.
Lema akihutubia maelfu ya wakazi wa jiji la Arusha huko Ngarenaro
Umati wa watu waliohudhuria mkutano huo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: