JENERALI ULIMWENGU AUNGANA NA TUNDU LISSU KUMTETEA MBOWE
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:33 PM
NA K-VIS BLOG
MWANDISHI mkongwe na
Mwanasheria, Jenerali Ulimwengu, leo Machi 2, 2017, ameonekana Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda
ya Dar es Salaam, akiwa kwenye jopo la mawakili wanaomtetea Mwenyekiti wa
CHADEMA, Freeman Mbowe, katika kesi ya Kikatiba aliyofungua kwenye mahakama hiyo akimlalamikia Mkuu wa Mkoa wa
Dar es Salaam, Paul Makonda, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,
Simon Sirro, na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Kanda hiyo, Camilius
Wambura.
Ulimwengu, ameungana na jopo la mawakili, Tundu Lissu, Peter Kibatala
na John Malya katika kumtetea Mbowe.
Aidha katika kesi hiyo
leo hii, Mahakama, imetupilia mbali maombi yaliyowasilishwa na Mbowe ya kutaka
asikamatwe hadi kesi yake ya msingi, itakapomalizika.
Maombi hayo yalitupwa kwa sababu kifungu cha sheria kilichotumika
kuyafungua si sahihi na kwamba hutumika pale ambapo sheria ziko kimya.
Uamuzi huo wa majaji umefikiwa kutokana na pingamizi la Jamhuri
lililowasilishwa na wakili mkuu wa serikali, Gabriel Malata kuiomba kuyatupilia
mbali maombi hayo kwani hayana msingi kisheria.
Mbowe amefungua kesi hiyo ya kikatiba namba 1, ya mwaka 2017 dhidi ya
wadaiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kamanda wa
Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam na Ofisa Upelelezi wa Makosa ya Jinai
Kanda Maalumu ya Dar es Salaam. Kesi hiyo itasikilizwa tena Machi 8, mwaka huu. Pichani juu, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe,
(kushoto), akitafakari jambo ndani ya Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam akiwa
na wakili wake Jenarali Ulimwengu (katikati) na Meya wa Ubungo Boniface Jacob
leo Machi 2, 2017.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: