IGAD; WAKIMBIZI WAHIFADHIWE KWA MUJIBU WA SHERIA ZA KIMATAIFA

mediaWaziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam DesalegnPhoto: Reuters/Tiksa Negeri
Mkutano wa IGAD umefunguliwa rasmi jumamosi jijini Narobi ambapo wito umetolewa na viongozi wa nchi wanachama wa shirika hilo kufanya kila wawezalo kuhakikisha kuwa wakimbizi wanapewa hifadhi bila kujali nchi wanazotoka.
Waziri mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Dusalegn alisisitiza wanachama kuwa wakimbizi lazima wahifadhiwe kwa vyovyote vile Kulingana na sheria za kulinda wakimbizi za kimataifa.
Hadi sasa raia wa Somalia wapatao Milioni mbili wameyakimbia makwao huku wengi wakiishi nchini Kenya, Ethiopia na nchini Uganda.
Umoja wa Mataifa umekuwa ukitoa wito kwa nchi za hasa Kenya kuendelea kuwapa hifadhi wakimbizi wa Somalia.

0 comments: