IGAD; WAKIMBIZI WAHIFADHIWE KWA MUJIBU WA SHERIA ZA KIMATAIFA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:06 AM
Waziri Mkuu wa Ethiopia Hailemariam DesalegnPhoto: Reuters/Tiksa Negeri
Mkutano
wa IGAD umefunguliwa rasmi jumamosi jijini Narobi ambapo wito umetolewa
na viongozi wa nchi wanachama wa shirika hilo kufanya kila wawezalo
kuhakikisha kuwa wakimbizi wanapewa hifadhi bila kujali nchi wanazotoka.
Waziri
mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Dusalegn alisisitiza wanachama kuwa
wakimbizi lazima wahifadhiwe kwa vyovyote vile Kulingana na sheria za
kulinda wakimbizi za kimataifa.
Hadi sasa raia wa Somalia wapatao Milioni mbili wameyakimbia makwao huku wengi wakiishi nchini Kenya, Ethiopia na nchini Uganda.
Umoja wa Mataifa umekuwa ukitoa wito kwa nchi za hasa Kenya kuendelea kuwapa hifadhi wakimbizi wa Somalia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: