BASI LA RUKSA CLASSIC LAGONGANA USO KWA USO NA GARI DOGO SHINYANGA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:13 AM
Basi la
RUKSA CLASSIC lenye namba za usajiri T 636 AWC likitoka jijini Mwanza
kwenda mkoani Kigoma limegongana uso kwa uso na gari dogo lenye namba za
usajiri T 210 DJJ katika kijiji cha Nhelegani mkabala na chuo cha
Ushirika Moshi kambi ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga.
Chanzo
cha ajali hiyo kimeeleza kuwa ajali hiyo iliyotokea majira saa nne asubuhi ni
uzembe wa dereva wa gari ndogo ambaye hakuwa na utulivu barabarani na
kujikuta yupo upande wa usiokuwa wake na kujikuta kugongana uso kwa uso na kusababisha ajali hiyo.
Hata
hivyo hakuna mtu aliyepoteza maisha ingawa dereva wa gari dogo na abiria
wake mmoja, wameumia na kukimbizwa katika hospitali ya rufaa mkoa wa
Shinyanga.
(PICHA ZOTE NA MASENGWA BLOG)
Basi likiwa limegongana uso kwa uso na gari dogo
Gari dogo likiwa limegongana na Basi hilo
Muonekano wa Basi hilo kwa nyuma
Muonekano wa mbele ya basi hilo
Wasamaria wakisaidia kulisogeza gari hiyo
Gari dogo likiwa likiwa katika muonekano huu
Watu wakishuhudia tukio hilo
Muonekano kwa Nyuma ya gari dogo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: