BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA KIGAMBONI LIMEPITISHA BAJETI YA MWAKA 2017-2018 YENYE VIPAUMBELE MBALIMBALI KWA MASLAHI YA WANANCHI WA WILAYA HIYO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:48 AM
Akivitaja
vipaumbele hivyo Mstahiki Meya wa Halmashauri hiyo ya Kigamboni Maabadi
Suleiman Hoja amesema bajeti hiyo itajikita zaidi kwenye kuongeza
ukusanyaji wa mapato kutoka bilioni 2 mpaka bilioni 8, halikadhalika
kuimarisha huduma za afya kwa kuongeza vifaa tiba, kupanua Zahanati,
kuboresha huduma za maji, kuboresha masoko na maeneo ya wafanyabiashara,
kuboresha sekta ya elimu kwa kuongeza madarasa, nyumba za walimu na
kurekebisha matundu ya vyoo, pia usafi wa mazingira wilaya hiyo utakuwa
moja ya vipaumbele kwenye bajeti hiyo.
Mstahiki
Meya Hoja ameongeza kuwa wanataraji kupokea bilioni 49 kutoka vyanzo
mbalimbali vya mapato ikiwemo ruzuku ya serikali, mapato ya ndani,
wafadhili na wananchi ambapo amesisitiza kuwa ilikufikia malengo
wanatakiwa watumie fursa zilizopo vizuri na kuongeza juhudi katika
ukusanyaji wa mapato.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: