USAJILI WA TIGO KILI HALF MARATHON 2017 JIJINI DAR ES SALAAM

 Katibu wa Kawe jogging Social and sport Club,  Seif Muhere akipokea tiketi za Kili marathon kutoka kwa Mwakilishi wa Tigo,  Viola Mboya kwa ajili ya ushiriki wa mashindano Tigo Kili Half Marathon 21Km, yanayotarajiwa kufanyika jumapili ijayo Tarehe 26 Februari  mkoani Kilimanjaro. Usajili huo ulifanyika jana Jumamosi Mlimani city jijini Dar es Salaam kwa kujisajili kwa kulipia kwa kutumia Tigopesa na zoezi  linaendelea leo siku ya jumapili.
Usajili unaendelea Mlimani City Jijini Dar es salaam.
Wananchi mbalimbali wakiendelea na Usajili wa mashindano ya Tigo Kili Half Marathon kwenye banda la Tigo jijini Dar es Salaam jana tayari kwa mashindano hayo yatakayofanyika tarehe 26 mwezi huu, Usajili huo ulifanyika kwa kutumia huduma ya Tigopesa, Zoezi la usajili linaendelea leo pia
Wananchi mbalimbali wakiendelea na Usajili wa mashindano ya Tigo Kili Half Marathon kwenye banda la Tigo Mlimani city  jijini Dar es Salaam jana tayari kwa mashindano hayo yatakayofanyika tarehe 26 mwezi huu Mkoani Kilimanjaro , Usajili huo ulifanyika kwa kutumia huduma ya Tigopesa.

0 comments: