Rais wa Marekani Donald Trump, anawazia kutoa amri nyingine mpya ya
kuwazuia raia kutoka baadhi ya nchi kuingia Marekani. Hii ni baada ya
amri aliyoitia saini kuzuiliwa na mahakama. Trump ametangaza kuwa kuna
uwezekeno wa amri nyingine mpya kutolewa siku ya Jumatatu au Jumanne
wiki ijayo ambayo haitowajumuisha wenye kumiliki kadi za kijani maarufu
kama 'green card' au wakaazi wa kudumu. Mkuu wa utumishi wa umma katika
Ikulu ya White House Reince Priebus aliwaambia wanahabari hapo jana
kuwa, kuiwasilisha kesi katika mahakama ya juu ni njia nyingine
wanayoweza kufikiria katika kutafuta utekelezwaji wa amri hiyo, ambayo
iliwapiga marufuku raia kutoka nchi 7 za Kiislamu kuingia Marekani.
TRUMP ATAFAKARI KUWASILISHA AMRI MPYA YA USAFIRI MAREKANI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:25 PM
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: