PAPAFRANCIS: MACHAFUKO NA UKATILI UKOMESHWE NCHINI KONGO DR

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis ametaka kuhitimishwa machafuko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Papa Francis aliyasema hayo jana Jumapili ambapo sanjari na kulaani kutumikishwa watoto kama askari nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, amewataka viongozi wa serikali ya Kinshasa kufanya haraka kwa ajili ya kuhitimisha vitendo vya ukatili nchini.
Watoto wadogo wanaotumikishwa kama askari
Katika shambulizi la hivi karibuni la wanachama wa kundi la kigaidi katika mkoa wa Kivu Kaskazini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwa akali watu 25 waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa pia limepasisha azimio la kutaka kuyanyang'anya silaha makundi ya wabeba silaha nchini humo.
Waasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hususan maeneo ya mashariki mwa nchi hiyo yamekuwa yakishuhudia hali ya mchafukoge kwa zaidi ya miaka 20 sasa kutokana na hujuma za makundi ya wabeba silaha.

0 comments: