MAMIA YA WAGENI WATIWA MBARONI NCHINI MAREKANI

Polisi wanaoshughulikia masuala ya wahamiaji nchini Marekani walianzisha opereseheni ya kushtukiza kuanzia siku ya Jumatatu hadi jana Ijumaa na kuwatia mbaroni mamia ya wahamiaji katika majimbo sita ya nchi hiyo.
Shirika la habari la Mehr limeripoti habari hiyo na kusema kuwa, hatua hiyo ya polisi wa Marekani imechukuliwa ikiwa ni kutekeleza amri wa Rais Donald Trump aliyoitoa tarehe 27 Januari mwaka huu ya kutaka kufuatiliwa kisheria mamilioni ya wahamiaji waishio nchini Marekani.
Polisi wa Marekani wanadai kuwa, lengo la operesheni hiyo ni kukabiliana na wahamiaji wahalifu, lakini operesheni hiyo inawajumuisha hata wahamiaji ambayo hawana historia yoyote ya kufanya uhalifu.
Ajenda kuu ya Rais Donald Trump wa Marekani ni kuwafukuza karibu wahamiaji milioni tatu waishio nchini humo.
Donald Trump, Rais wa Marekani mwenye chuki na wageni hususan Waislamu.

Majimbo yasiyopungua sita ya Marekani yameshuhudia uvamizi wa polisi dhidi ya wahamiaji na miongoni mwa miji kulikofanyika operesheni hiyo ni Chicago, New York na Los Angels. Katika majimbo ya Carolina Kaskazini na Carolina Kusini nako kumefanyika operesheni hiyo kali ya  kuwatia mbaroni wahamiaji.
Amri ya tarehe 27 Januari ya Donald Trump iliweka vikwazo vingi pia dhidi ya wahamiaji kutoka nchi saba za Waislamu za Iran, Iraq, Sudan, Somalia, Libya, Syria na Yemen. Hata hivyo hatua hiyo imekumbwa na malalamiko makubwa ndani na nje ya Marekani kutokana na kwenda kinyume na hata katiba ya nchi hiyo.

0 comments: