Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa (wa tatu kulia) akitazama sukari na nishati ya kuni
inayotengenezwa kwa kutumia makapi ya miwa inayokamuliwa katika kiwanda
cha sukari cha Manyara wakati alipotembelea kiwanda hicho jana Februari 19 2017. Kuni hizo zina ubora unaofanana na ule wa makaa ya mawe na
hutumika zaidi katika mitambo inayotumia nishati ya kuni. Kulia ni
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Tizeba na wa nne kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dkt. Joel Bendera. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa wilaya mstaafa, Mama Sanka
baada ya kuwasili kwenye makazi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara mjini
Babati akiwa katika ziara ya mkoa huo, Februari 19, 2017.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa (wa tatu kushoto) akitazama sanamu ya binadamu wakati alipotembelea
moja ya darasa la Chuo cha Uuguzi katika hospitali ya Haydom wilayani
Mbulu
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa (wa pili kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mtafiti katika
hospitali ya Haydom wilayani Mbulu, Rosemary Mshama (kulia) wakati
alipotembelea Kituo cha Utafiti cha hospitali hiyo .
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa (wa kwanza kulia) akifurahia ngoma ya asili ya kabila la Wahatzabe
wakati alipowasili kwenye hospitali ya Haydom kuanza ziara ya wilaya ya
Mbulu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: